Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2017

PUTIN AWAFUKUZA WANADIPLOMASIA 755 WA TRUMP

Putin aagiza wanadiplomasia 755 wa Marekani kuondoka Urusi Sambaza habari hii Facebook   Sambaza habari hii Twitter   HakiAFPImageKufukuzwa wa wanadiplomasia hao kutapunguza idadi hadi 455 Rais wa Urusi Vladimir Putin ameagiza wafanyakazi 755 wa ubalozi wa Marekani nchini Urusi kusitisha shughuli zao kufikia Septemba mosi mwaka huu. Urusi imeidhinisha hatua hiyo kwa ghadhabu kufuatia vikwazo vipya vilivyopitishwa na bunge la Marekani dhidi yake, kwa tuhuma za kuingilia uchaguzi wa taifa hilo mwaka jana. Marekani kwa upande wake, inasema imesikitishwa na uamuzi huo, na inapima athari na kutafakari namna ya kujibu hatua hiyo Marekani yawafukuza wanadiplomasia 35 wa Urusi Bunge la wawakilishi Marekani launga mkono vikwazo dhidi ya Urusi Hatua hii ya Urusi imekuja baada ya vikwazo vipya dhidi ya Urusi kuidhinishwa kwa wingi wa kura na mabunge yote ya congress nchini Marekani Jumanne, licha ya kwamba Ikulu ya White house ilipinga kura hiyo. Rais huyo wa Urusi

MFANYABIASHARA MAARUFU NCHINI AFARIKI DUNIA

 #MWANANCHI Mfanyabiashara huyo anamiliki vitega uchumi mbalimbali mkoani hapa ikiwemo hoteli za kitalii za Impala, Naura na Ngurdoto Mountain Lodge. Mfanyabiashara maarufu nchini, Maleu Mrema amefariki dunia jana akiwa kwenye matibabu nchini Afrika Kusini. Akizungumza na Mwananchi ndugu wa marehemu,Vincent Laswai alithibitisha msiba huo akiwa nyumbani kwa marehemu eneo la Uzunguni jijini Arusha. Akihojiwa na gazeti hili Laswai amesema kwamba alipokea taarifa za kifo cha marehemu jana saa 12 jioni na uongozi wa familia utatoa taarifa za kifo cha mfanyabiashara huyo leo. Laswai, amesema kwamba ni mapema kuzungumzia chanzo cha kifo kwa sababu bado hawajapata taarifa kutoka katika hospitali aliyokuwa akitibiwa nchini humo. Hivi karibuni marehemu Mrema alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya ambapo Juni mwaka huu alipelekwa Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu.

KESI YA WABUNGE 8 CUF INATATANISHA.

KESI YA WABUNGE 8 CUF BADO NI NGANGALI . Waraka wa BASHIR YAKUB. +255784482959 Ili wafanikiwe walitakiwa kutumia nafasi kuu tatu. Mosi kufungua kesi na kuzuia kikao cha nidhamu cha Cuf . Pili kufungua kesi kuizuia tume ya uchaguzi kuidhinisha kufutwa na uteuzi wabunge wapya. Tatu  kufungua kesi kulizuia bunge kuwaapisha wabunge wapya wateule. 1.KUZUIA  KIKAO CHA NIDHAM CHA CUF . Kesi nzuri ilitakiwa kufunguliwa mara tu baada ya kupata wito wa kikao cha nidhamu. Hapa wangeweza kufungua kesi kwa hati ya dharula na kufanya maombi madogo ya zuio la muda(temporally injunction). Wangezuia kikao cha nidhamu cha Cuf  na katu  kisingefanyika. 2. KUIZUIA TUME YA UCHAGUZI. Lakini kama wangeshindwa kuzuia kikao cha Cuf pengine kwa kuchelewa ama vinginevyo  bado walikuwa na nafasi ya kufungua kesi na kuomba zuio dhidi ya Tume ya uchaguzi  kuidhinisha kufutwa kwao kwa mujibu wa Ibara 78(4) ya katiba  inayosomwa na kifungu cha 86(8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi. Wangeomba zuio la kuz

KUKU ALIYEPELEKWA KWA MGANGA AZALIWA NA MCHEPUKO

Mdada ajifungua kuku huko Zimbabw e Mchepuko a.k.a Demu, alinogewa na penzi la mume wa mtu, Akaamua kwenda kwa Kalumanzila a.k.a.mganga wa jadi ili apate limbwata kali la kupora mume wa mtu...akaambiwa apeleke kuku ili kutengeneza hilo limbwata wakafanikiwa  kulisuka hilo limbwata. Sasa Mwenye mume a.k.a mke wa mtu,akashtukia mchezo mzima na yeye akaenda kwa mganga wa jadi mwingine ili kutegua limbwata hilo akafanikiwa. Kilichotokea ni yule Mchepuko a.k.a mwizi wa waume za watu kunasa mimba. baada ya miezi 9 akaenda hospitali kujifungua akitegemea kumzalia mtoto buzi wake. Sasa huko hospitali akazaa kuku yuleyule kuku aliyempeleka kwa mganga ili kutengeneza limbwata limbwata limedunda limbwata limemrudia. Hilo ni tukio la kweli,...na unaweza kuona polisi nao walifika kutuliza amani kwenye picha nyingine,na kuku aliyezaliwa akiwa kwenye sahani,pamoja na pamba za madokta walizotumia kwenye zoezi la kujifungua huyo mchepuko...   Imeletwa kwenu  na ripota wetu huko Zimbabwe

KIJANA MHITIMU WA CHUO WA MIAKA 22 AMLAWITI MSICHANA WA MIAKA 11 NIGERIA

Kijana wa miaka 22 na mhitimu wa chuo cha Abia State Nigeria faculty ya Historia alikamatwa Jana mchana akiwa anambaka msichana wa miaka 10. Kijana huyu kabla hajafanya kitendo hicho, mnamo mda wa saa 8 mchana alipita nyumbani kwa baba yake na kumsalimia na kuulizia kuhusu biashara za baba yake zinaendaje, kisha akaondoka kuelekea kwake, kabla hajafika kwake alipita nyumbani kwa msichana yule aliyebakwa na kumsalimia........... Baba wa kijana huyu ni Fundi wa kutengeneza Samani za ndani. Kijana huyu alimwambia msichana yule kuwa amemnunulia kandambili mpya kisha akamwambia waende wote chumbani kwake ili akampatie, na walipofika hakumpatia kqnfambili hizo alianza kumshikashika msichana yule kwenye mwili wake na kisha kuanza kumlazimisha kufanya tendo la ngono bila ridhaa yake. Mtuhumiwa alikamatwa na vijana majirani zake waliosikia kelele za msichana yule. Kijana huyu wa miaka 22 akithibitisha kufanya kitendo hicho kiovu alisema ni kweli alimbaka msichana yule. Katika upelelezi il

ACACIA WAKOSA GAWIO LA FAIDA-BASHE ASEMA

HUSSEIN BASHE ASHANGAA MCHANGA KUWAPA HASARA ACACIA. "Mheshimiwa Rais, naomba nikupe taarifa - tarehe 21 Julai, Mkurugenzi Mtendaji wa ACACIA ametangaza kuwa shareholders wa ACACIA hawatawalipwa gawio kwa sababu cashflow yao imepungua kwa asilimia 80% kufuatia uamuzi wako wa kuzuia makontena ya makinikia. Hivyo hawatalipwa hadi ufumbuzi wa makontena hayo utakapopatikana. "Sasa najiuliza mbona walisema ule mchanga tu na wala hauna thamani? Sasa iweje leo makapi yawe na thamani ya asilimia 80% kiasi cha kufanya shareholders wakose gawio?" Mh Hussein Bashe Mbunge - Nzega Mjini (CCM) (akiongea kwenye mkutano wa hadhara wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli mkoani Tabora)

KUTANA NA MAAJABU YA MIAYO, MACHOZI, NA MENGINE MENGI

MAMBO 8 YA KUSHANGAZA YANAYOFANYWA NA MWILI WAKO KUKULINDA PASIPO WEWE KUJUA. Mwili wa binadamu unafanya mambo mengi ya kibaiolojia ambayo mara nyingi ni vigumu kuyaelewa. Mwili una mifumo mbalimbali ya ulinzi ambayo inatulinda na hatari zinazoweza kutudhuru. Mifumo hiyo inatulinda masaa 24 ya siku, Siku zote 7 za wiki, katika mambo yote yanayoweza kuhatarisha maisha yetu. Yafuatayo ni mambo yanayofanywa na mwili  ambayo ni kati ya hiyo mifumo ya ulinzi wa mwili wa binadamu. 1. KUPIGA MIAYO (YAWNING) Lengo kubwa la kupiga muayo ni kuupoza ubongo baada ya joto kuzidi kwenye ubongo au baada ya ubongo kuchoka kufanya kazi. Vile vile kama ukiwa umechoka au una njaa husabababisha oxygen kupungua kwenye damu na kwenye mapafu, hii hupelekea tatizo la kupumua, hivyo kupiga miayo husaidia kuingiza oxygen ya ziada mwilini ili irudishe mwili katika hali yake ya kawaida. 2. KUPIGA CHAFYA (SNEEZING) Mara nyingi tunapiga chafya pale pua zetu zinapokua zimejaa bakteria wa magonjwa ambao hawah

TCU YAFUNGA VYUO 19 KUHAKIKI UBORA WA ELIMU

TCU imevifunga Breki Vyuo Vikuu 19 Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imesema kuwa imefanya uhakiki wa vyuo vyote vya elimu ya juu nchini ili kuhakiki ubora wa elimu inayotolewa vyuoni hapo, ripoti ya uhakiki huo ilionyesha mapungufu kadhaa katika baadhi vyuo. Hivyo tume imeamua kuchukua uamuzi wa kusitisha udahili wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/18 kwa vyuo hivyo. Aidha, Tume hiyo imevitaja vyuo hivyo kuwa ni pamoja na:     1. Eckenforde Tanga University     2. Jomo Kenyatta University, Arusha     3. Kenyatta University, Arusha     4. United African University of Tanzania     5. International Medical and Technological University (IMTU)     6. University of Bagamoyo     7. Francis University College of Health and Allied Sciences     8. Archibishop James University College     9. Archibishop Mihayo University College     10. Cardinal Rugambwa Memorial University College     11. Kampala International University Dsm College     12. Marian University

USHAURI WA HASHIMU RUNGWE KWA TUNDU LISSU

Hashim Rungwe amshauri Tundu Lissu kumpuuza Zitto Kabwe Mwenyekiti wa chama cha Sauti ya UMMA Hashim Rungwe amemuomba Rais wa Chama cha Sheria Tanganyika Tundu Lissu kumpuuza Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe. Rungwe amesema alishangazwa na kejeli alizomwaga Zitto Kabwe dhidi ya Lissu ambaye kwa sasa ndiye mwanasiasa tishio zaidi nchini. Rungwe amesema Zitto kama alikuwa anapinga msimamo wa Chadema angepaswa kutoa hoja na siyo mipasho aliyotoa. Kiongozi huyo aliyegombea Urais mwaka 2015 amesema alichokisema Tundu Lissu ndiyo msimamo wa mpinzani yeyote wa kweli nchini.Amesema na ndiyo sababu CCM wote wamemshangilia Zitto na sasa wanamuona ni mwenzao. Rungwe amemshauri Tundu Lissu kumpuuza Zitto Kabwe kwani kujibizana naye inaweza kuwa mkakati wa CCM wa kupunguza mashambulizi dhidi yake. Rungwe amemalizia kwa kusema nchi nyingi za Afrika watawala wamepandikiza wapinzani bandia na vibaraka ili kutawala muda mrefu.

KAIMU KATIBU MKUU UVCCM AMEMBIPU LISSU

SHAKA: TUNDU LISSU AMECHOKA MAISHA YA URAIANI "Tumemtafakari na kubaini ana nia ya kuwania urais mwaka 2020, anachotaka ni kuwaacha kwenye mataa jamaa zake kina Lowasa na sumaye, ila ajue akizidi kueneza matamshi ya kipuuzi anaweza kukamatwa na kutupwa mahali" -  Shaka  "Lisu si kama papai ambalo kama likiwekwa ndani litaooza na kuharibika, anaweza kukaa huko kwa usalama wake na wa nchi, tumeruhusiwa kisheria kufanya siasa za vyama vingi kwa ustaarabu na uungwana na si kufanyiana kejeli na dhihaka " - Shaka "Lisu ni nani mbele ya mamlaka za kisheria na kikatiba, tunadhani anataka nyingi nasaba hivyo ajiandae siku yoyote anaweza kukutwa na msiba, msiba wa kujitakia hauna pole, dola yoyote haifanani na kitambaa cha deki" - Shaka "Ujasiri wa kuidhihaki mamlaka ya Rais ni sawa na mtu juha au punguani anayejaribu kutupa jiwe katikati ya mzinga wa nyuki au mpumbavu kumchezea simba sharubu " - Shaka Shaka H. Shaka ni Kaimu Katibu Mkuu UVCCM

LEO KATIKA AFYA YAKO: TANGO LINA FAIDA GANI?

Tango ni tunda moja wapo yenye maji mengi kama vile tikiti maji ,linabeba virutubisho vingi vitamin K,B,C,potasium,manganese .  Tango lina polyphenols ambayo inasaidia kukuepusha kupata maradhi sugu.Ni vizuri mkatumia matanga mara kwa mara kwa kutengeneza juice,kuchanganya kwenye kachumbali (salad)bila kumenya  maganda yake yanabeba virutubisho vizuri,au unaweza weka kwenye mkate na kuchanganya na maji ya kunywa kuyapa ladha na vitamin   Umuhimu wa kula tango kwa afya yako   1.Kuipa kinga ubongo Tango lina anti-inflammatory flavonol inayopelekea kuipa kinga ubongo na kukufanya kuwa na kumbukumbu nzuri (improve your memory).   2.Kupunguza hatari ya kupata cancer. Tango linakupunguzia hatari ya kuapata cancer ya maziwa na shemu za uzazi (uterine,mayai ya uzazi (ovari).   3.Kutoa harufu mbaya mdomoni. Kata kipande cha tango weka mdomoni kwa dakika 5 fanya mara 3 kwa siku inataidia kutoa bakteria wafanya kunuka mdomo .   4.Kupunguza stress Tango linavitamins B,vitaminB1 vi

ZITTO KABWE AMJIBU TUNDU LISSU

ZITTO KABWE AMJIBU TUNDU LISSU "Huu ni uhayawani. Hii ni nchi huru. Kukaribisha wageni kuingilia mambo yetu ni upuuzi na umazwazwa. Tupambane ndani kuleta demokrasia. NDANI" - Zitto Kabwe "Kama hamtaki kuambiwa ukweli shauri yenu. Ni upuuzi mkubwa kutaka nchi ikatiwe misaada. Ni kasumba ya kikoloni. Ni ujinga usiovumilika" - Zitto Kabwe "Nataka maendeleo ya watu wetu. Uwekezaji kutoka nje na misaada ni sehemu tu ya juhudi. Mwanasiasa anayetaka nchi inyimwe misaada ni muflisi" - Zitto Kabwe "Napinga ujinga popote. Leo unamkaribisha mgeni akusaidie Kwa kukata misaada. Ukiingia madarakani si utampa dhahabu yote? Kasumba hovyo kbs" - Zitto Kabwe "Ndio uuze uhuru wa nchi yako? Misaada Kuwa fimbo Kwa nchi zetu ni jambo la kishamba Sana. Misaada ikikatwa anaumia nani? JPM? Lisu?" - Zitto Kabwe "Hakuna kupingana. Ninapinga ujinga. Siasa za kukatiwa misaada ni siasa za kizamani, ushamba na kasumba ya kutawaliwa" - Zitto kabwe &q

HASARA YA PUNYETO AU MASTURBATION

... JINSI PUNYETO (MASTURBATION) INAVYOATHIRI SUALA LA NGUVU ZA KIUME. 0687744030 Kama wewe upo kwenye mitandao mbali mbali ya kijamii utakuwa umeshaona jinsi magroup ya mambo ya picha za uchi na video za ngono yalivyo mengi kuanzia instagram facebook na WhatsApp. Washiriki wengi hasa vijan wengi a, na tafiti mbali mbali zinaonyesha k wengi uwa wanaathiriwa sana na picha hizo na kuchochewa kujichua (kupiga punyeto) ili kumaliza hamu zinazoamshwa na hisia kali za ngono baada ya kutazama picha hizo na vidoe hizo. Wengi wao hawafahamu namna gani suala hilo (masturbation) linavyoweza kuathiri afyaya uzazi hasa nguvu za kiume. Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Of course ipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi ya kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishi

FAIDA 30 ZA ALOE VERA MWILINI

FAIDA ZA MMEA WA ALOE VERA (Mshubiri): Mshubiri ni mti wenye Miujiza ya kutibu maradhi sugu kama ugonjwa wa Saratani (Cancer) ugonjwa wa Kisukari Diabetis, Ugonjwa wa cholesterol, ugonjwa wa kuvimba sehemu ya mwili na magonjwa mengine mengi. Tuone faida za mmea wa aloe vera au mshubiri 1. Huondoa uvimbe katika jicho Weka kiasi kidogo cha majimaji ya mu-aloe vera freshi kisha kuamka asubuhi, acha kwa dakika kadhaa kisha jisafishe. Uvimbe lazima ukimbie. Pia unaweza kuloweka pamba katika majimaji ya mualoe vera na kisha jisafishe katika jicho lenye uvimbe. 2. Huzuia na kuondoa michirizi ya tumbo itokanayo na ujauzito Anza kwa kupakaa majimaji ya mualoevera juu ya tumbo lako na ufanye kama masaji hivi taratibu juu ya tumbo mara 2 kwa siku katika kipindi chote cha ujauzito na baada ya kujifungua kwa miezi michache mpaka michirizi ipotee yote. 3. Hutibu bawasiri Ile ile sifa moja iliyonayo ya kutibu uvimbe ambayo inaweza pia kutibu malengelenge na uvimbeuchungu kwenye mwako wa mwili

UMUHIMU WA FIGO KWA BINADAMU

UMUHIMU WA FIGO. Figo zina majukumu muhimu sana katika mwili wa binadamu- kwanza inaondoa sumu kutoka mwili wa binadamu na kusafisha damu na kutoa sumu zote. Kama figo haifanyi kazi vizuri, basi hii inaweza kusababisha mkusanyiko wa sumu katika mwili na inaweza kusababisha baadhi ya matatizo makubwa ya afya. Dalili za mwanzo za ugonjwa wa figo na jinsi ya kuweka figo zako katika afya nzuri. Figo inafanya kazi nyingi muhimu katika mwili wa binadamu. 1.Kuweka katika uwiano mzuri kiwango cha maji. Figo ina uwezo wa kusawazisha kiwango cha maji katika mwili wa binadamu,na pia inashiriki katika kutoa kemikali kwa njia ya mkojo. 2.Kutoa taka mwilini. Sisi sote tunajua moja ya kazi kuu za figo ni kusafisha mwili, kutoa sumu,chumvi na urea. 3.Kusimamia kanuni za damu. Kama kiwango cha oksijeni kitakuwa chini katika figo, itasababisha kuundwa kwa erythroprotein, homoni ambayo inachochea marrow katika mifupa(bone marrow). 4.Kusimamia Kanuni za asidi. Hii ni muhimu

WIZI WA PIKIPIKI WAWAPONZA, WATATU WACHOMWA MOTO MPAKA KUFA HUKO KAHAMA

* Picha : Watu Watatu Wauawa Kwa Kuchomwa Moto Kwa Wizi Wa Pikipiki Kahama * Wananchi waliojichukulia sheria mkononi jana  wamewaua kwa kuwachoma moto watu watatu ambao majina yao bado hayajafahamika katika kijiji cha Kitwana kata ya Busoka wilayani Kahama,mkoani Shinyanga kwa tuhuma za wizi wa pikipiki. Kwa mujibu wa mashuhuda, mauaji ya mtu wa kwanza yalifanywa majira ya saa nane usiku wa kuamkia jana baada ya kutokea wizi wa pikipiki, huku watu wengine wawili wakiuawa jana  majira ya saa nne asubuhi. Inaelezwa kuwa mtuhumiwa wa kwanza alipokamatwa aliwataja wenzake wawili waliouawa jana baada ya kuvunja nyumba ya mmoja wao na kukuta pikipiki tatu zimehifadhiwa kwenye shimo. Afisa mtendaji wa mtaa wa Kitwana, Peter Joseph amekiri kutokea kwa tukio hilo huku akilaani vikali kitendo cha wananchi kujichulia sheria mkononi, na kuwataka kuacha tabia hiyo kwani ni kinyume cha sheria. Miili ya marehemu hao ilichukuliwa na Jeshi la polisi wilaya ya Kahama, na kupelekwa katika chum

WAZIRI MKUU AMWAGIZA MWAKYEMBE ALICHUNGUZE BARAZA LA MICHEZO TANZANIA (BMT)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe alifanyie mapitio Baraza la Michezo Tanzania (BMT) na iwapo hatoridhika na utendaji wake alivunje. “Ninamuagiza Waziri mwenye dhamana kufanya mapitio na kutathmnini upya utendaji kazi wa Baraza la Michezo Tanzania juu ya usimamizi wake wa  michezo nchini na kama hataridhika, anayo mamlaka ya kulivunja Baraza hilo.” Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Julai 5, 2017) katika hotuba yake ya kuahirisha Mkutano wa Saba wa Bunge mjini Dodoma. Amesema Serikali ya Awamu ya Tano haitafumbia macho usimamizi mbovu na utawala wa michezo usiojali maslahi ya Taifa. “Serikali imeazimia kuimarisha utendaji kwa vyombo vya michezo nchini ili kila mwenye dhamana awajibike ipasavyo.” Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameipongeza timu ya vijana walio chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys iliyoshiriki na kutoa upinzani mkubwa kwenye mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani

RC PAUL MAKONDA AZAWADIWA GARI NA KAMPUNI YA UTENGENEZAJI WA MAGARI

RC MAKONDA AKABIDHIWA WINGLE 5 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mh. Paul Makonda leo asubuhi amekabidhiwa zawadi ya gari aina ya *Double Cabin Wingle 5 kutoka kwa kampuni ya watengenezaji wa magari ya  *Great Wall Motor Company* ya Afrika Kusini ikishirikiana na kampuni ya wauzaji Magari ya *Kifaru Motors* ya Tanzania. Akiongea katika makabidhiano hayo mkurugenzi wa *Great Wall Motor Company* ukanda wa Kusini mwa Afrika *Bwana Jianguo Liu* alisema kuwa zawadi hiyo ni ishara ya kampuni hiyo kutambua jitihada mbalimbali  za ofisi ya mkuu wa Mkoa na watumishi wake wanazofanya katika kutumikia wananchi na kusaidia kuboresha utendaji kazi. Katika salamu za shukrani *Mh. Makonda* alishukuru uongozi mzima wa kampuni ya *Great Wall* ukishirikiana na wauzaji *Kifaru Motors* kwa kutambua jitihada za ofisi yake na kuahidi kuendelea kuwatumikia wananchi wa Dar es salaam kwa moyo na kutimiza falsafa ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania *Mh. Dr John Pombe Magufuli* ya *"HAPA KAZI TU"

KOREA KASKAZINI WASEMA KOMBORA LA MASAFA MAREFU LINA UWEZO WA KUFIKA POPOTE DUNIANI HATA HUKO MAREKANI LITAFIKA

Korea Kaskazini yatamba yasema Kombora lao linauwezo wa kufika Marekani  Korea Kaskazini ilitoa picha za kombora hilo la masafa marefu ICBM likirushwa Marekani imethibitisha kwamba Korea kaskazini ilifanyia jaribio kombora la masafa marefu ambalo kulingana na wataalama wanaamini linaweza kufika Alaska Marekani. Waziri wa maswala ya kigeni amelitaja jaribio hilo kuwa vitisho vipya kwa Marekani na dunia na kuonya kwamba Washington haitakubali hatua ya Korea Kaskazini kujihami na nyuklia. Pyongyang imedai siku ya Jumanne kwamba ilifanikiwa kulifanyia majaribi kombora lake la masafa marefu ICBM. Wakijibu, Marekani na Korea Kusini zilirusha makombora kusini mwa maji Korea. Zoezi hilo la kijeshi la pamoja lililenga kuonyesha uwezo wa mashambulizi ya mataifa hayo mawili, Pentago imesema. Ijapokuwa jaribio la Jumanne lilionekana kuwa hatua kubwa ,wataalam wanaamini kwamba Korea kaskazini haina kombora la masafa marefu la kinyuklia. Bwana Tillerson pia alionya kwamba taifa lolote amba

ACACIA:BAADA YA MARUFUKU YA MAKINIKIA WAAMUA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MAREKANI

Ni baada ya kupatwa na pigo kubwa  Baada ya Serikali ya Tanzania kuweka zuio la kutosafirisha Makinikia Kampuni  ya Acacia, jana ilitangaza kufungua 'kesi' ya kuomba upatanishi wa mgogoro unaoendelea baina yake na serikali. Taarifa iliyotolewa jana na Acacia ilisema kampuni hiyo imewasilisha taarifa hiyo ya kutafuta upatanishi kwa niaba ya kampuni zake tanzu za Bulyanhulu Gold Mine Limited (BGML) na Pangea Minerals Limited (PML), inayomiliki mgodi wa Buzwagi. Kampuni hiyo ya Uingereza inamiliki pia mgodi wa dhahabu wa North Mara, lakini ni miwili hiyo ambayo mali yake huhusisha uchenjuaji wa makinikia. Migogoro ya kimataifa ya kiuwekezaji hutatuliwa na ama Kituo cha Kimataifa cha Utatuzi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) au Chemba ya Kimataifa ya Biashara (ICC). Ingawa taarifa ya Acacia haikueleza imefungua wapi ombi lake la kutaka upatanishi wa mgogoro wa makinikia, chanzo cha kuaminika kiliiambia pande hizo mbili zitaketishwa pamoja ICSID yenye makao yake makuu Washingt

JPM ASEMA HATAKI KWENDA NJE YA NCHI

 Rais John Magufuli amesema amepata mialiko zaidi ya 60 kwenda nje ya nchi baada ya kuwa Rais lakini ameikataa kwa sababu anataka kuishughulikia Tanzania kwanza. “Niende nje kufanya nini wakati ntaenda tu nikishastaafu, nataka nimalize kwanza haya ya hapa ndani,” alisema. Ameyasema hayo jana (Jumanne Julai 4) wakati akihutubia wakazi wa Sengerema katika uzinduzi wa mradi wa maji Sengerema. Rais Magufuli amesema hana haja ya kwenda nje ya nchi kwa sababu bado ana mzigo mkubwa wa kumaliza ufisadi.

NAIBU SPIKA: WAPINZANI HAWAJUI KUZICHANGANUA HOJA LICHA YA UWASILISHAJI WAO MZURI

 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson. Naibu spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt.  Tulia Ackson  amefunguka na kusema wabunge wa upinzani muda mwingine huwa wanaleta hoja nzuri kwa serikali lakini serikali inashindwa kuzipokea hoja hizo kutokana na uwasilishaji wao. Naibu Spika amesema hayo leo Dodoma wakati akifanyiwa mahojiano katika kipindi cha bunge, ambapo alikuwa akitoa mtazamo wake juu ya bajeti kuu ya serikali kwa mwaka 2017/2018 "Wabunge wa upinzani muda mwingine wanaleta hoja nzuri sana bungeni lakini tatizo kubwa linakuja katika lugha inayotumika inakuwa si lugha ya staha ndiyo maana unaona hata serikali inakuwa haikubali. Bunge ni jumba la kisiasa, hivyo kila mwamba ngoma huvutia kwake, upande wa chama kinachoongoza ndiyo chenye serikali wana namna yao ya kuishauri serikali, ila wale ambao wanataka kuingia madarakani nao wana namna yao ya uchangiaji bungeni ndiyo maana kuna kuwa na mvutano wa hapa na pale&quo

FAIDA ZA MBEGU ZA MAPERA KWA AKINA MAMA WOTE

Miujiza ya mbegu za pera kwa kinamama WAWEZA kuita ni miujiza. Wakati walaji wengi wa mapera wakiwa na kawaida ya kuondoa mbegu, imefahamika kuwa kufanya hivyo ni kosa kubwa kiafya kwa sababu wahusika hujikosesha faida nyingi kiafya. Uchunguzi  unaohusisha mahojiano na madaktari pamoja na maandiko mbalimbali ya utafiti wa lishe, umebaini kuwa ulaji wa mbegu za mapera, iwe kwa kuzisaga na kunywa kupitia juisi au hata kuzimeza bila kuziponda zina manufaa na zina miujiza mingi katika kuukinga mwili dhidi ya magonjwa. Baadhi ya virutubisho vilivyomo kwenye pera na pia mbegu za tunda hilo ni pamoja na kiwango cha juu cha vitamin A, vitamin C, vitamin E na madini yakiwamo ya niacin, thiamine, chuma, calcium, potassium, phosphorus na manganese. Pia kuna kiasi kikubwa cha kinga dhidi ya vijisumu. Faida zake mwilini ni pamoja na kupunguza uwezekano kwa mlaji kupata saratani ya tezi dume; kisukari; saratani ya matiti; maradhi ya shinikizo la damu; tumbo kuvimba kwa sababu ya chakula kutos

MAGONJWA YA ZINAA NA DALILI ZAKE

Magonjwa ya zinaa na dalili zake Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdia, kankroidi, utando mweupe , Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Shida kubwa ya magonjwa mengi ya zinaa ni kwamba dalili zake hazionekani kwa urahisi na kama yasipotibiwa kikamilifu yanaweza kuleta madhara makubwa. Maelezo kuhusu magonjwa ya zinaa yaliyoenea sana ni kama yafuatayo: *Kisonono* : Huchukua muda wa siku 1 hadi 14 tangu kuambukizwa mpaka kuonyesha dalili za kuumwa. Kwa wanawake dalili za kisonono ni maumivu chini ya tumbo ambayo yanaweza kuambatana na homa na kutokwa uchafu ukeni. Wapo wanawake wengine ambao hawaoni dalili zozote. Kwa wanaume dalili ni kutokwa na usaha uumeni na kupata maumivu wakati wa kukojoa. Athari yake kwa mwanamke ni kuziba mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, na vilevile ugumba. Kwa mtoto aliye tumboni mwa mama mjamzito kisonono cha mama yake kinaweza kusababisha upofu. Kwa mwanaume athari

AFISA WA POLISI ANAYEICHEZEA TIMU YA BLACK STARS YA GHANA

Afisa   wa   polisi   anayeichezea  Black Stars ya Ghana Haki miliki ya pichaSAMUEL SARFOImage captionSamuel Sarfo kushoto ambaye alikuwa mlinzi sasa ni mchezaji mahiri wa Black Stars Mwaka mmoja uliopita Samuel Sarfo afisa wa polisi nchini Ghana alipigwa picha , akiwalinda wachezaji wa timu ya soka ya taifa kabla ya mechi ya kimataifa. Miezi 12 baadaye Sarfo mwenyewe ameichezea The Black Stars kwa mara ya kwanza akiingizwa kama mchezaji wa ziada katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Marekani katika mechi ya kirafiki iliochezwa mjini Connecticut siku ya Jumamosi. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 pia ni nahodha wa klabu ya ligi ya taifa hilo Liberty Proffessionals na anachanganya uchezaji wake wa soka na kazi zake kama afisa wa polisi. Mengi yamebadilika tangu aonekane na mavazi ya polisi , akilinda kikosi cha taifa na kama alivyomwambia mwandishi wa BBC Afrika Nishat Ladha ana mengi ya kumshukuru mwajiri wake. Alisema kuwa anatimizi ndoto yake ya kuichezea timu ya taifa. ''

UGONJWA WA BAWASIRI NA TIBA ZAKE

UJUE UGONJWA WA (hemorrhoid) kuota kinyama sehemu ya haja kubwa . Maada hii ni muhimu sana maana ni tatizo linalowatesa watu wengi ungana nami hapa uweze kupata elimu pia . Bawasirini (kuota kinyama sehemu ya haja kubwa) ni uvimbe wa mishipa ya damu kwenye njia ya haja kubwa. Huonekana kutuna au kujaa kama jipu karibu na unyeo. Inaweza kutoa muwasho, hisia ya kuungua, au maumivu; hasa wakati wa kujisaidia. Wakati mwingine bawasiri hupasuka na kutoa damu kidogo nyekundu inayong’aa kwenye kinyesi. Bawasiri ni tatizo la kawaida wakati wa ujauzito na miongoni mwa watu wanaokaa au kubeba mizigo mikubwa kutwa nzima, lakini kila mtu anaweza kuupata. Maumivu kutokana na bawasiri huzidi zaidi mgonjwa anapokuwa na tatizo la choo kigumu, kwa sababu kukitoa choo kigumu hulazimisha mishipa kwenye njia ya haja kubwa kupanuka zaidi. bawasiri zipo za aina mbili. 1 Aina inayotembea (Yaani ikitoka ndani na kurudi) 2 Aina inayosimama VISABABISHI VYA BAWASIRI (KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUB

DAWA YA ASILI NA USAFI KWA WANAWAKE NI MUHIMU

Dawa ya Uchafu Ukeni Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano. Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’. Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla. Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni: • Kuwa na wapenzi wengi • Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango • Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali • Uchafu • Uvutaji sigara • Pombe • Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni Dalili: • Kutokwa na uchafu usio wa kawaida • Kutokwa na uchafu wenye harufu kali kama s