Skip to main content

KOREA KASKAZINI WASEMA KOMBORA LA MASAFA MAREFU LINA UWEZO WA KUFIKA POPOTE DUNIANI HATA HUKO MAREKANI LITAFIKA

Korea Kaskazini yatamba yasema Kombora lao linauwezo wa kufika Marekani

Korea Kaskazini ilitoa picha za kombora hilo la masafa marefu ICBM likirushwa

Marekani imethibitisha kwamba Korea kaskazini ilifanyia jaribio kombora la masafa marefu ambalo kulingana na wataalama wanaamini linaweza kufika Alaska Marekani.

Waziri wa maswala ya kigeni amelitaja jaribio hilo kuwa vitisho vipya kwa Marekani na dunia na kuonya kwamba Washington haitakubali hatua ya Korea Kaskazini kujihami na nyuklia.

Pyongyang imedai siku ya Jumanne kwamba ilifanikiwa kulifanyia majaribi kombora lake la masafa marefu ICBM.

Wakijibu, Marekani na Korea Kusini zilirusha makombora kusini mwa maji Korea.
Zoezi hilo la kijeshi la pamoja lililenga kuonyesha uwezo wa mashambulizi ya mataifa hayo mawili, Pentago imesema.

Ijapokuwa jaribio la Jumanne lilionekana kuwa hatua kubwa ,wataalam wanaamini kwamba Korea kaskazini haina kombora la masafa marefu la kinyuklia.

Bwana Tillerson pia alionya kwamba taifa lolote ambalo linasaidia kiuchumi na kijeshi Korea kaskazini ama limefeli kuidhinisha kwa ukamilifu maamuzi ya baraza la usalama ya Umoja wa Mataifa linasaidia utawala hatari.

Marekani imetaka kufanyika kwa mkutano wa dharura wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kujadili swala hilo.

Mkutano wa faragha wa wanachama wa baraza hilo unatarajiwa baadaye siku ya Jumatano.

Je Korea kaskazini ilisema nini siku ya Jumanne?

Tangazo hilo katika runinga ya taifa ya Korea kaskazini lilisema kuwa kombora hilo aina ya Hwasong -14 linaloweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine lilisimamiwa na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.

Ilisema kuwa kombora hilo liliruka umbali wa kilomita 2,802 na kusafiri kwa umbali wa kilomita 933 kwa dakika 39 kabla ya kuanguka baharini.

Korea Kaskazini imesema kuwa ni taifa lililojihami kinyuklia ambalo linamiliki kombora la masafa marefu linaloweza kushambulia eneno lolote duniani.

Marekani na Korea Kaskazini nini kimebadilika?

Chombo cha habari cha Korea kaskazini KCNA baadaye kilimnukuu Kim jong un akisema kuwa jaribio hilo ni zawadi kwa Wamerakani siku yao ya uhuru.

Jaribio hilo ambalo ni miongoni mwa majaribio ya makombora yake linakiuka marufuku ya baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.

Lakini wataalam wengi wanaamini kwamba Pyongyang bado haijakuwa na uwezo wa kutengeza kichwa cha kinyuklia kinachoweza kutosha katika kombora la masafa marefu na kwamba kombora kama hilo haliwezi kushambulia eneo linalolenga.

Je kombora hilo lina uwezo wa kusafiri umbali gani?

Swala kuu ni linaweza kusafiri kwa umbali gani, alisema mwandishi wa BBC Evans Seoul.
Je linaweza kushambulia Marekani?.

David Wright , kutoka muungano wa kisayansi anasema kuwa iwapo ripoti hiyo ni ya sawa ,kombora hilo linaweza kusafiri kwa umbali wa kilomita 6.700.

''Umbali huo unaweza kulifanya kufika Alaska, lakini sio visiwa vya Hawaii ama hata majimbo mengine 48 ya Marekani'',alisema.

''Sio kombora pekee ambalo Korea Kaskazini itahitaji'', mwandishi huyo anasema.

Pia ni lazime iwe na uwezo wa kulinda kichwa cha nyuklia kinapopaa angani na sio wazi iwapo Korea kaskazini ina uwezo huo.

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA ASILI NA USAFI KWA WANAWAKE NI MUHIMU

Dawa ya Uchafu Ukeni Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano. Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’. Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla. Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni: • Kuwa na wapenzi wengi • Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango • Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali • Uchafu • Uvutaji sigara • Pombe • Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni Dalili: • Kutokwa na uchafu us...

FAIDA ZA MAZIWA YA SOYA MWILINI

DONDOO ZA AFYA........!!!! MAAJABU YA SOYA MWILINI. MAAJABU YA SOYA MWILINI. Soya ni zao la jamii ya mikunde lenye aina nyingi za matumizi; ni zao linalofaa kwa chakula cha binadamu na wanyama na pia ni zao la biashara. Zao hilo lina kiasi kingi cha protini yenye ubora wa hali ya juu kuliko kiasi kilichopo katika aina nyingine ya mazao ya mimea.ZK  taasisi inayojishughuliza na uzalishaji wa bidhaa za vyakula lishe na mimea na matunda, vinavyoweza kutiba magonjwa mbalimbali wamezalisha maziwa ya Soya ambayo yana  kiasi cha protini inayozidi hata kiasi cha protini katika nyama, mayai na maziwa. Hii inamaanisha kuwa maziwa ya soya ni chanzo rahisi na cha bei nafuu cha protini hasa kwa watu wenye kipato kidogo ambao hawawezi kumudu gharama za vyanzo vingine vya protini kama nyama, maziwa na samaki. Aidha, maziwa ya soya yanaa mafuta bora yasiyo kuwa na lehemu (cholesterol). Uwingi na ubora wa protini katika maziwa ya soya yanaweza kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto na kuwao...

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...