Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2018

Hiki ndicho chanzo cha Kifo cha Agnes Masogange

Agnes Gerald amefariki leo muda wa mchana alipokuwa akitibiwa katika hospitali ya Dokta Ngoma Jijini Dar es Salaam. Agnes alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kupungukiwa damu na ugonjwa wa mapafu.  Agnes Gerald (Masogange) ni Model na Video Queen wa muda mrefu sana Tanzania. Aliwahi kufanya ngoma na mwanamziki Belle 9 Masogange kutokea kwenye huo wimbo Belle 9 alimpatia jina hilo la Masogange. Kutokea kwenye wimbo huo Agnes Gerald alipata umaarufu mkubwa sana Tanzania kwenye Tasnia ya mziki. Learn more, then put them in mind, live it!

Kigogo wa Bandari Prosper Kimaro Asomewa Mashtaka Leo

Leo April 19, 2018 Meneja wa Fedha wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Prosper Kimaro amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na kosa la kujilimbikizia mali zenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.4 zisizolingana na kipato chake halali. Kimaro anadaiwa kumiliki nyumba zenye thamani ya Bilioni 1,178,370,334, zilizopo maeneo ya Temeke DSM na magari 7 yenye thamani Shilingi Milioni 307,364,678.20. Kimaro amesomewa mashtaka yake na wakili wa serikali, Vitalis Peter mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambapo amedai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na kosa moja. Wakili Vitalis amedai mshtakiwa anakabiliwa na kosa la kujilimbikizia mali zisizolingana na kipato chake ambapo anadaiwa amelitenda kosa hilo kwa miaka tofauti kati ya 2012 na 2016. Anadaiwa mali hizo amejilimbikizia maeneo ya Temeke DSM akiwa mtumishi wa umma wa TPA kama Meneja wa Fedha, amekutwa na mali zisizolingana na kipato chake halali cha zamani na cha sasa. Mali hizo ni nyumba 2 zilizopo mtaa wa Uwazi

Mke wa Bush afariki dunia.  

Washington, Marekani. Barbara Bush, mke wa aliyekuwa rais wa zamani wa Marekani na mwanaharakati amefariki akiwa na umri wa miaka 92. Ndiye aliyekuwa nguzo ya kisiasa ya marais wawili wa Taifa hilo, George HW Bush ambaye ni mumewe na mwanawe George W Bush. Barbara aliyekuwa mke wa rais mwaka 1989 hadi 1993 aalikuwa mgonjwa kwa kwa muda mrefu na alikataa kupatiwa matibabu. Rambirambi zimekuwa zikitumwa nchini Marekani kutoka maeneo mbalimbali duniani. Mumewe George HW Bush ana miaka 93. Mtoto wake George W Bush aliingia madarakani mwaka 2000 na kuongoza mihula miwili akiwa Rais wa 43 wa Marekani. "Mama yangu mpendwa ametuacha akiwa na umri wa miaka 92. Laura, Barbara, Jenna nami tunaomboleza lakini roho zetu zimepumzika kwa sababu tunajua yake pia imepumzika," amesema George W Bush katika rambirambi zake.

UINGEREZA NA UFARANSA KUSHAMBULIA NCHINI SYRIA BILA YA IDHINI YA UMOJA WA MATAIFA.

KISA CHA MAREKANI UINGEREZA NA UFARANSA KUSHAMBULIA NCHINI SYRIA BILA YA IDHINI YA UMOJA WA MATAIFA. Mapema 14 April 2018 Marekani Uingereza na Ufaransa zilifanya mashambulizi ya kijeshi nchini Syria zikitumia ndege za kivita. Habari toka vyombo mbalimbali vya habari vililipoti kuwa jumla ya makombora 103 yalivyatuliwa yakiwa yamelenga maeneo mbalimbali lakini makombora 71 yalinduguliwa angani na majeshi ya Syria kabla hayajagonga sehemu yaliyokuwa yamelengeshwa. Vifaa vya ulinzi vya anga vilivyotumika kuyadungua makombora yaliyokuwa yamerushwa na Ndege za Marakani na washirika wake ni Vifaa vya ulinzi wa anga vya Urusi aina S-200. Hata hivyo vifaa hivi vya S-200 ni vifaa vya nyuma sana kwani Urusi kwa sasa ina vifaa vingine bora zaidi ambavyo ni S-300 S-400 na S-500 ambavyo havikutumika kujikinga na mashambulizi haya ya Marekani Uingereza na Ufaransa nchini Syria. Baada ya mashambulizi haya ambayo hayakuwa na madhara makubwa kutokana na makombora mengi kuripuliwa yakiwa hayajagonga

Diwani na Msanii Baba Levo Ampiga Daktari Kisa Vibarua

​ MSANII BABA REVO AMBAYE NI DIWANI AMPIGA DAKTARI KISA KUCHELEWA KUWALIPA VIBARUA ​ Diwani wa Kata ya Mwanga Kaskazini  Mkoani Kigoma Revokatus Kipando maarufu kwa jina la Baba Levo amemdhalilisha kwa kumpiga Dk. wa Zahanati ya  Msufini iliyoko mkoani kigoma   kwa kosa la kuchelewesha kuwalipa vibarua waliokua wanafanya ukarabati katika zahanati  hiyo. Daktari huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema diwani alifika nakuanza kumdhalilisha na kumkashifu kwa kuchelewesha kuwalipa wafanyakazi hao  mbele ya wagonjwa  na kusababisha wagojwa kuondoka pasipo kutibiwa. “Amefika  hapa kwa kufoka, kunitukana , kufanya vurugu ofisini na kanipiga, kisa pesa zilizo nje ya uwezo wangu ambazo zilikua na utaratibu za kufuatiliwa lakini hataki kufuata taratibu za kazi amehatalisha amani ya maisha yangu  na hii siyo mara ya kwanza na yuko kinyume cha sheria,” alisema Daktari huyo. Kwa mjibu wa mashuhuda wa tukio hilo akiwemo  Muuguzi wa Hospitali wa zamu  ambaye jina lake limehif

Mwanafunzi Ajikata Uume Baada ya Kuambiwa na Mpenzi Wake Kuwa Ana Kibamia

Mwanafunzi wa Kichina alikata sehemu zake za siri baada ya mpenzi wake kumdhihaki kwa kuwa na uume mdogo. Footage inaonyesha huyo kijana asiyevaa chochote lakini T-shirt, amesimama kimya nje ya Chuo cha Guangdong Peizheng kusini mashariki mwa China. Wanafunzi wengi walikusanyika ili kuchukua picha na video za kijana huyo. Chuo sasa kimeingia ili kujaribu kuchunguza na kuachana na uvumi unaozunguka kwenye vyombo vya habari vya kijamii. Majadiliano moja ya vyombo vya habari vilieleza kuwa mwanafunzi huyo alichukua hatua kali baada ya kuambiwa na mpenzi wake kuwa ana uume mdogo. Mpenzi wake alidai yeye alijihusisha mwenyewe baada ya mwanamke mdogo asiyejulikana kutoa maoni yasiyofaa juu ya mrithi wake. Mvulana huyo alisema kuwa "alichanganyikiwa", lakini hakuna habari zaidi juu ya hali yake ya sasa. Chuo hakikuweza kuthibitisha kwa nini aliamua kujiumiza mwenyewe.  Kwa kauli fupi kuthibitisha kwamba alikuwa amejijeruhi mwenyewe na kwamba alipelekwa hospital

Man cuts off genitals after girlfriend mocked his ‘small penis’

A CHINESE student chopped off his genitals after his girlfriend mocked him for having a small penis. Footage shows the young man wearing nothing but a T-shirt, calmly standing outside Guangdong Peizheng College in south-eastern China. Many students flocked to take photographs and film the man who was later rushed to hospital. The college has now stepped in to try and stop rumours circulating on social media. One social media conversation suggested the student took drastic measures after arguing with his girlfriend. Another claimed he castrated himself after an unidentified young woman made disparaging comments about his endowment. The young man was said to be in a "sober state of mind", but there is no further information about his current condition. The college could not confirm why he decided to hurt himself. In a brief statement confirming that he had injured himself and that he was taken to hospital after the college was notified about what had happened. This har

8 ways to stop loving someone who doesn’t love you back

Falling in love with someone is one of the most thrilling things that can happen to a person, but only when those feeling are appreciated. Unrequited love can become a dangerous illness that will lower your self-esteem and make you feel like you don’t deserve happiness at all. Fortunately, there is a cure for this illness and as hard as it may sound, un-loving the person that’s making you suffer so much is the only way to become truly free again. After all, everyone just wants to be happy, that includes you and your partner. If you’re feeling that your relationships are inevitably coming to an end and bring you nothing but pain, or if you’ve fallen for the person that doesn’t care about you at all, here are 8 sure ways to get on with your life. 1. Accept the fact he’s not right for you Whether it’s actual experience you share together or simply your wishful thinking getting the best of you, just acknowledge the fact that he’s not the one. It becomes much easier after that! Stop decei

UN yasimama kidete dhidi ya vita vya Syria

UN nayo haijanyamazia hatua hizi zinazoendelezwa na wababe wa dunia Kutokana na kuongezeka kwa hali ya wasiwasi kuhusu mvutano huo wa Syria, mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa utafanyika baadae leo. Mkutano huo utakuwa wa faragha. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema hadi sasa Baraza la Usalama la umoja huo limeshindwa kufikia makubaliano ya kidiplomasia kuhusu Syria na amezitaka nchi wanachama wa kudumu wa baraza hilo kufikiria upya kwa kina na kuchukua hatua zitakazofaa ambazo hazitaongeza zaidi makali katika mzozo wa Syria. Nchi hizo ni pamoja na Marekani, Urusi, China, Ufaransa na Uingereza. Urusi na Marekani hadi sasa zimepiga kura ya turufu kupinga azimio la kila mmoja la kutaka kuanzisha uchunguzi wa kimataifa kuhusu matumizi ya silaha za sumu. Jana jioni Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Jim Mattis pamoja na Mkurugenzi wa Shirika la Ujasusi la Marekani, CIA, Mike Pompeo walikutana katika Ikulu ya Marekani kujadiliana kuhusu hali ya

Vita vya Syria Mbioni Kusababisha Vita Ya Tatu ya Dunia. Marekani na Urusi Hawaelewani Tena!

VITA vinavyoendelea nchini Syria vilivyodumu kwa miaka mitano sasa viko mbioni kuiingiza dunia yetu katika Vita Vikuu vya Tatu vya Dunia. Wakubwa wa Dunia yetu, Marekani na Urusi, wanaonekana kutofautiana kwa kiasi kikubwa ambapo sasa Marekani anasema hataki tena mazungumzo na mwenziwe Urusi kuhusu suluhisho la mgogoro wa Syria kwa njia ya amani bali anaangalia "Njia Mbadala" ya kumaliza mgogoro huo. Je, njia hiyo ni ipi? Urusi yeye anadai yupo nchini Syria kwa mwaliko wa Rais Bashar Al Assad ili kumsaidia kupambana na makundi ya kigaidi yanayotishia utawala wake. Marekani kwa upande wake anaunga mkono kundi linalojiita Free Syrian Army kwa lengo la kumng'oa Rais Bashar Al Assad madarakani, ingawa wachambuzi wa mambo wanadai makundi yote ya kigaidi yanayopigana nchini Syria dhidi ya serikali ya Rais Bashar Al Assad, likiwemo kundi la Al Qaeda, yaliundwa na yanafadhiliwa na Marekani na nchini nyingine za Magharibi. Urusi tayari ina zana za kutosha nchini Syria yakiwemo m

Magufuli amkumbuka Moringe Sokoine kwa mambo aliyofanya nchini.

​Leo ni Kumbukumbu ya Kifo cha Edward Moringe Sokoine.......Tazama Hapa Alichokiandika Rais Magufuli​ Ikiwa leo ni Kumbukumbu ya Kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine aliyefariki dunia Aprili 12, 1984 kwa ajali ya gari, eneo la Dakawa nje Kidogo ya Mji wa Morogoro, Rais Dkt. John Magufuli amefunguka na kueleza alivyomfahamu kiongozi huyo enzi za uhai wake na mchango wake katika Taifa letu.  Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Magufuli amesema; “Katika siku kama ya leo tarehe 12 Aprili 1984 nikiwa Mpwapwa JKT nikitumikia jeshi langu “Oparesheni Nguvukazi” tukatangaziwa kifo cha marehemu Edward Moringe Sokoine, ilikuwa siku ya majonzi shujaa huyu niliyemjua na kumshabikia ikawa siku yake ya mwisho. “Wakati tunapoazimisha siku kama hii ya kifo chake, watanzania tuige mfano wake kwani alikuwa msema kweli, asiyeogopa, mpiga vita rushwa,ufisadi, unyonyaji,mzalendo wa kweli na aliyechukia

Matibabu ya Lissu: Bunge Lamkataa Tena. Soma habari kwa kina hapa!

Spika Ndugai atoa ufafanuzi juu ya matibabu ya Tundu Lissu.   Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amesema utaratibu wa Bunge kugharamia matibabu ya Tundu Lissu unaendelea kufanyiwa kazi na ukikamilika utatolewa ufafanuzi. Spika Ndugai ametoa kauli hiyo Jana Alhamisi Aprili 5, 2018 wakati akihojiwa na Kituo cha Televisheni  hapa nchini ikiwa ni siku moja kupita tangu aliporejea nchini akitokea India kwa matibabu. Mhe Tundu Lissu ambaye ni mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya Chadema alishambuliwa kwa risasi zaidi ya 30, Septemba 7, 2017 na kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na siku hiyohiyo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi ambako alilazwa hadi Januari 6 alipohamishiwa Ubelgiji katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven, anakoendelea na matibabu. Tangu wakati huo, familia yake na viongozi wa Chadema wamekuwa wakililalamikia Bunge kutogharamia matibabu ya mbunge huyo huku Lissu naye mara kadhaa akizungumzia jambo hilo. Lakini katika mahojiano hayo

MLIMA KILIMANJARO MBIONI KULIPUKA SASA

BREAKING NEWS:  The crater on top of  Mt Kilimanjaro started smoking  yesterday and is about to erupt any time now.  The smoke can be sighted from as far as Voi and Moshi. The earth crack spotted in Mai Mahiu Kenya is aligned with the mountain and the fissure is expected to widen all the way to the Mountain. Upon eruption, hot earth and molten rocks shall shoot miles in the air then rain down on surrounding areas.  The crack will be at least ten miles wide and will swallow land, farms, animals and anybody in the area. Urgently alert your friends and family who live around Arusha, Moshi, Namanga and  all the way to Mai Mahiu. URGENT.