Skip to main content

Kigogo wa Bandari Prosper Kimaro Asomewa Mashtaka Leo

Leo April 19, 2018 Meneja wa Fedha wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Prosper Kimaro amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na kosa la kujilimbikizia mali zenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.4 zisizolingana na kipato chake halali.

Kimaro anadaiwa kumiliki nyumba zenye thamani ya Bilioni 1,178,370,334, zilizopo maeneo ya Temeke DSM na magari 7 yenye thamani Shilingi Milioni 307,364,678.20.

Kimaro amesomewa mashtaka yake na wakili wa serikali, Vitalis Peter mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambapo amedai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na kosa moja.

Wakili Vitalis amedai mshtakiwa anakabiliwa na kosa la kujilimbikizia mali zisizolingana na kipato chake ambapo anadaiwa amelitenda kosa hilo kwa miaka tofauti kati ya 2012 na 2016.

Anadaiwa mali hizo amejilimbikizia maeneo ya Temeke DSM akiwa mtumishi wa umma wa TPA kama Meneja wa Fedha, amekutwa na mali zisizolingana na kipato chake halali cha zamani na cha sasa.

Mali hizo ni nyumba 2 zilizopo mtaa wa Uwazi Temeke (Mil 124.2), kiwanja kimoja kilichopo Yombo Vituka (Mil.12.9), nyumba 2 zilizopo Temeke (Mil 63.5).

Pia nyumba nyingine 3 zilizopo Temeke zenye thamani ya (Mil.159), nyumba nyingine 3 zilizopo maeneo hayo (Mil 170.1), nyumba nyingine moja (Mil 71.3).

Pia ana kiwanja Temeke (Mil 35), kiwanja kingine (Mil 25) na kujenga nyumba 3 (Mil 159), pia nyumba nyingine moja (Mil 106), pia nyumba nyingine 3 zilizopo Temeke zikiwa na thamani ya (Mil 214).

Pia ana nyumba 4 zilizopo Viziwa Ziwa Kibaha Mjini (Mil 199.7), nyumba nyingine Kilimahewa Tandika (Mil 70).

Pia anamiliki magari aina ya Toyota Land cruise (Mil 180.1), Mitsubishi (Mil 38.4), Massey Ferguson (Mil.24), Trailer (Mil 4.5), Toyota Harrier (Mil 35.8), Trailer (Mil 4.8), Massey Ferguson (Mil 19.1).

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshtakiwa alikana makosa yake ambapo Wakili Vitalis amedai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, pia hana pingamizi na dhamana.

Hakimu Simba ametoa masharti ya dhamana kwa mshtakiwa kuwa na wadhamini 2 watakaowasilisha hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya Sh.Mil 200, pia mshtakiwa asitoke nje ya mkoa wa Dar es Salaam bila kibali pamoja na kuwasilisha hati zake za kisafiria.

Mshtakiwa huyo hajatimiza masharti ya dhamana, ambapo Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi May 3,2018.

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

FAIDA ZA MAZIWA YA SOYA MWILINI

DONDOO ZA AFYA........!!!! MAAJABU YA SOYA MWILINI. MAAJABU YA SOYA MWILINI. Soya ni zao la jamii ya mikunde lenye aina nyingi za matumizi; ni zao linalofaa kwa chakula cha binadamu na wanyama na pia ni zao la biashara. Zao hilo lina kiasi kingi cha protini yenye ubora wa hali ya juu kuliko kiasi kilichopo katika aina nyingine ya mazao ya mimea.ZK  taasisi inayojishughuliza na uzalishaji wa bidhaa za vyakula lishe na mimea na matunda, vinavyoweza kutiba magonjwa mbalimbali wamezalisha maziwa ya Soya ambayo yana  kiasi cha protini inayozidi hata kiasi cha protini katika nyama, mayai na maziwa. Hii inamaanisha kuwa maziwa ya soya ni chanzo rahisi na cha bei nafuu cha protini hasa kwa watu wenye kipato kidogo ambao hawawezi kumudu gharama za vyanzo vingine vya protini kama nyama, maziwa na samaki. Aidha, maziwa ya soya yanaa mafuta bora yasiyo kuwa na lehemu (cholesterol). Uwingi na ubora wa protini katika maziwa ya soya yanaweza kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto na kuwao...

Supplements During Pregnancy: What’s Safe and What’s Not

AUTHORITY NUTRITION Evidence Based Supplements During Pregnancy: What’s Safe and What’s Not Pregnancy can be one of the most exciting and happy experiences in a woman’s life. However, it can also be a confusing and overwhelming time for some mothers-to-be. The internet, magazines and advertisements flood women with advice on how to stay healthy during pregnancy. While most women know that high-mercury seafood, alcohol and cigarettes are off-limits during pregnancy, many are unaware that some vitamins, minerals and herbal supplements should be avoided as well. Information on which supplements are safe and which aren’t often varies between sources, making things more complicated. This article breaks down which supplements are believed to be safe to take during pregnancy and explains why some supplements must be avoided. Why Take Supplements During Pregnancy? Consuming the right nutrients is important at every stage of life, but it’s especially crit...