Skip to main content

UINGEREZA NA UFARANSA KUSHAMBULIA NCHINI SYRIA BILA YA IDHINI YA UMOJA WA MATAIFA.

KISA CHA MAREKANI UINGEREZA NA UFARANSA KUSHAMBULIA NCHINI SYRIA BILA YA IDHINI YA UMOJA WA MATAIFA.

Mapema 14 April 2018 Marekani Uingereza na Ufaransa zilifanya mashambulizi ya kijeshi nchini Syria zikitumia ndege za kivita. Habari toka vyombo mbalimbali vya habari vililipoti kuwa jumla ya makombora 103 yalivyatuliwa yakiwa yamelenga maeneo mbalimbali lakini makombora 71 yalinduguliwa angani na majeshi ya Syria kabla hayajagonga sehemu yaliyokuwa yamelengeshwa. Vifaa vya ulinzi vya anga vilivyotumika kuyadungua makombora yaliyokuwa yamerushwa na Ndege za Marakani na washirika wake ni Vifaa vya ulinzi wa anga vya Urusi aina S-200. Hata hivyo vifaa hivi vya S-200 ni vifaa vya nyuma sana kwani Urusi kwa sasa ina vifaa vingine bora zaidi ambavyo ni S-300 S-400 na S-500 ambavyo havikutumika kujikinga na mashambulizi haya ya Marekani Uingereza na Ufaransa nchini Syria.

Baada ya mashambulizi haya ambayo hayakuwa na madhara makubwa kutokana na makombora mengi kuripuliwa yakiwa hayajagonga sehemu yaliyokuwa yamelengeshwa na mengine kukosa shabaha Urusi imekitaja kitendo hivyo kama cha uharifu kwa Taifa huru la Syria.Eidha Urusi haijaamua kujibu mashambulizi haya kwa kile inachoamini Syria kwa sasa ni Salama baada ya Waasi Waliokuwa wakipewa silaha na nchi za magharibi kushindwa vita na kuondoka kwa magubaliano maalumu.

Urusi haijajibu mashambulizi kwa kujua nia ovu ya mataifa haya yanayotafuta kuona Syria ikiendelea kuwa sehemu ya vita hadi Rais wa nchi hiyo aondoke madarakani.

Urusi haijajibu mashambulizi kwa kuangalia maslahi mapana ya maisha ya watu wa Syria ambao wanahitaji mda wa kupumzika baada ya miaka 6 ya vita.

Urussi haijajibu mashambulizi hayo kwa kuangalia maslahi mapana ya kuepusha vita vya tatu vya dunia ambavyo vinaweza kuathiri maslahi ya Urussi hasa katika kipindi hiki ambacho miezi michache Mashindano ya kabumbu ya kombe la Dunia ambayo yataanza nchini Urusi hivi karibuni.

Kwa Upande wa Marekani Rais Trump aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter  kuwa "Kazi imekamilika" huku akiwapongeza washirika wake ambao ni Uingereza na Marekani.

Hata hivyo Rais Trump na Washirika wake wamepata upinzani mkali toka ndani na nje ya Marekani kwa mashambulizi hayo ambayo hayakuwa na kibali cha Umoja wa mataifa lakini pia yakionekana kama uonevu kwani hapakuwa na visibitisho vya wazi kama serikali ya Syria ilitumia silaha za kemikali kwa raia wake.Huku wachunguzi wa masuala ya kisiasa wakihoji kwa nini rais Bashar Al Assad atumie silaha za kemikali kwa watu wake huku vita vikiwa vimemalizika.

Kwa Upande wa gharama za mashambulizi hayo ya mda mfupi  kizikadiliwa ni zaidi ya dollar za marekani $60,000,000 ikiwa gharama ya kombora moja ni zaidi ya dollar $500,000 pasipo gharama za mafuta ya ndege n.k

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA ASILI NA USAFI KWA WANAWAKE NI MUHIMU

Dawa ya Uchafu Ukeni Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano. Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’. Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla. Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni: • Kuwa na wapenzi wengi • Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango • Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali • Uchafu • Uvutaji sigara • Pombe • Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni Dalili: • Kutokwa na uchafu us...

FAIDA ZA MAZIWA YA SOYA MWILINI

DONDOO ZA AFYA........!!!! MAAJABU YA SOYA MWILINI. MAAJABU YA SOYA MWILINI. Soya ni zao la jamii ya mikunde lenye aina nyingi za matumizi; ni zao linalofaa kwa chakula cha binadamu na wanyama na pia ni zao la biashara. Zao hilo lina kiasi kingi cha protini yenye ubora wa hali ya juu kuliko kiasi kilichopo katika aina nyingine ya mazao ya mimea.ZK  taasisi inayojishughuliza na uzalishaji wa bidhaa za vyakula lishe na mimea na matunda, vinavyoweza kutiba magonjwa mbalimbali wamezalisha maziwa ya Soya ambayo yana  kiasi cha protini inayozidi hata kiasi cha protini katika nyama, mayai na maziwa. Hii inamaanisha kuwa maziwa ya soya ni chanzo rahisi na cha bei nafuu cha protini hasa kwa watu wenye kipato kidogo ambao hawawezi kumudu gharama za vyanzo vingine vya protini kama nyama, maziwa na samaki. Aidha, maziwa ya soya yanaa mafuta bora yasiyo kuwa na lehemu (cholesterol). Uwingi na ubora wa protini katika maziwa ya soya yanaweza kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto na kuwao...

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...