Skip to main content

Vita vya Syria Mbioni Kusababisha Vita Ya Tatu ya Dunia. Marekani na Urusi Hawaelewani Tena!

VITA vinavyoendelea nchini Syria vilivyodumu kwa miaka mitano sasa viko mbioni kuiingiza dunia yetu katika Vita Vikuu vya Tatu vya Dunia. Wakubwa wa Dunia yetu, Marekani na Urusi, wanaonekana kutofautiana kwa kiasi kikubwa ambapo sasa Marekani anasema hataki tena mazungumzo na mwenziwe Urusi kuhusu suluhisho la mgogoro wa Syria kwa njia ya amani bali anaangalia "Njia Mbadala" ya kumaliza mgogoro huo. Je, njia hiyo ni ipi?

Urusi yeye anadai yupo nchini Syria kwa mwaliko wa Rais Bashar Al Assad ili kumsaidia kupambana na makundi ya kigaidi yanayotishia utawala wake. Marekani kwa upande wake anaunga mkono kundi linalojiita Free Syrian Army kwa lengo la kumng'oa Rais Bashar Al Assad madarakani, ingawa wachambuzi wa mambo wanadai makundi yote ya kigaidi yanayopigana nchini Syria dhidi ya serikali ya Rais Bashar Al Assad, likiwemo kundi la Al Qaeda, yaliundwa na yanafadhiliwa na Marekani na nchini nyingine za Magharibi.

Urusi tayari ina zana za kutosha nchini Syria yakiwemo makombora yake ya kujihami ya S-400 kwa ajili ya kulinda anga. Vivyo hivyo Marekani nayo inadaiwa kupeleka silaha nchini Syria kupitia kwa makundi ya kigaidi.

Mapigano makali kwa sasa yanaripotiwa jijini Aleppo kati ya majeshi ya Assad na yale ya kigaidi, wote wakigombea umiliki wa mji huo.

Je, kivipi mgogoro huo unaweza kugeuka vita vya dunia? Kutokana na wakubwa hawa wawili Marekani na Urusi kuwa na masilahi yanayokinzana katika ardhi ya Syria yanayohusisha matumizi ya silaha, upo uwezekano mkubwa wa mgogoro huo kuwa wa dunia nzima. Hivi sasa Vladimir Putin anaonekana kuutawala uwanja wa mapigano nchini Syria kitendo ambacho Marekani hawatakubali kuona wakishindwa na kuaibishwa! Watakapoamua kuingilia kati moja kwa moja kwa kutuma askari wake na silaha zake, hapo ndipo patakuwa patamu maana Urusi naye hatakuwa na njia nyingine bali kuingia kimoja Syria na ikizingatiwa kwamba Urusi wana "ka historia ka kushinda vita japo kwa mbinde"; mfano, mwaka 1812 waliwanyuka Ufaransa na wakati wa WWII (1939 - 1945) tena wakawanyuka Wajeremani wa Hitler.

Kama inavyofahamika, Marekani ni mjumbe wa NATO, hivyo kuingia kwa marekani nchini Syria kupigana, kutamaanisha kundi la NATO kuingia vitani. Kwa upande wake Urusi, naye anao washirika wake kama China na Iran na wengine. Ikifikia hatua hiyo, nchi kama Korea ya Kaskazini inaweza kutumia mwanya huo kushambulia masilahi ya Marekani popote pale itakapoona panafaa.

Pale Mashariki ya Kati penyewe hapaeleweki hata kidogo -- Marekani iko na Israel na Saudi Arabia; Urusi ndiyo hivyo tena iko na Iran, Syria yenyewe, na Uturuki kwa mbali japo nayo ni ndumilakuwili.

Cha kutisha zaidi kuhusu wakubwa hawa kuingia vitani, ni silaha za kisasa na hatari zaidi, zikiwemo za Nyuklia wanazozimiliki, ambazo wakiamua kuzitumia basi ni majanga tupu.

Kwa habari zaidi bonyeza hapa

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

Ndege ya Ukraine yaanguka Iran ikiwa na abiria 180, Abiria wote wafariki

Ndege ya Ukraine aina ya Boeing-737 iliyokuwa na abiria 180 imeanguka Iran, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo. Watoa huduma wa msalaba mwekundu wa Iran wanasema kuwa hakuna dalili yeyote kama kuna mtu aliyepona katika ajali hiyo. Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la kimataifa la ndege la Ukraine ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari katika uwanja wa ndege wa Imam Khomeini mjini Tehran. Ripoti za awali zinadai kuwa ndege hiyo ilikuwa safarini kuelekea mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.  Haijabainika ikiwa ajali hiyo ina uhusiano wowote na mzozo wa Iran-na Marekani. Kikosi cha uokoaji tayari kimetumwa katika eneo la tukio karibu na uwanja wa ndege, eneo ambalo ndege lilianguka. Credit: GettyImage " Ndege imeshika moto na tumetuma kikosi huko ... ," kiongozi wa huduma za dharura Pirhossein Koulivand,ameviambia vyombo vya habari ambapo Reuters imeripoti. Je tutegemee machafuko zaidi kutokea? Endelea kuwa pamoja nasi bega kwa bega, mshirikishe na mwenz...