Skip to main content

AFISA WA POLISI ANAYEICHEZEA TIMU YA BLACK STARS YA GHANA

Afisa wa polisi anayeichezea Black Stars ya Ghana

Haki miliki ya pichaSAMUEL SARFOImage captionSamuel Sarfo kushoto ambaye alikuwa mlinzi sasa ni mchezaji mahiri wa Black Stars

Mwaka mmoja uliopita Samuel Sarfo afisa wa polisi nchini Ghana alipigwa picha , akiwalinda wachezaji wa timu ya soka ya taifa kabla ya mechi ya kimataifa.

Miezi 12 baadaye Sarfo mwenyewe ameichezea The Black Stars kwa mara ya kwanza akiingizwa kama mchezaji wa ziada katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Marekani katika mechi ya kirafiki iliochezwa mjini Connecticut siku ya Jumamosi.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 pia ni nahodha wa klabu ya ligi ya taifa hilo Liberty Proffessionals na anachanganya uchezaji wake wa soka na kazi zake kama afisa wa polisi.

Mengi yamebadilika tangu aonekane na mavazi ya polisi , akilinda kikosi cha taifa na kama alivyomwambia mwandishi wa BBC Afrika Nishat Ladha ana mengi ya kumshukuru mwajiri wake.

Alisema kuwa anatimizi ndoto yake ya kuichezea timu ya taifa.

''Ni ndoto iliotimia.Hiyo ni ndoto ya kila kinda kuvaa jezi za timu ya taifa nchini Ghana''.

Amesema kuwa kiungo wa kati Emmanuel Agyemang-badu ambaye alipiga picha naye akivalia magwanda yake ya polisi na ambaye hakuchaguliwa katika timu hiyo dhidi ya Marekani amekuwa akimsadia sana.

Anasema kuwa anataka kucheza soka ya kulipwa kwa sababu ulimwengu unafaa kuona mchezo wake.

Source #BBCswahili

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA ASILI NA USAFI KWA WANAWAKE NI MUHIMU

Dawa ya Uchafu Ukeni Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano. Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’. Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla. Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni: • Kuwa na wapenzi wengi • Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango • Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali • Uchafu • Uvutaji sigara • Pombe • Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni Dalili: • Kutokwa na uchafu us...

FAIDA ZA MAZIWA YA SOYA MWILINI

DONDOO ZA AFYA........!!!! MAAJABU YA SOYA MWILINI. MAAJABU YA SOYA MWILINI. Soya ni zao la jamii ya mikunde lenye aina nyingi za matumizi; ni zao linalofaa kwa chakula cha binadamu na wanyama na pia ni zao la biashara. Zao hilo lina kiasi kingi cha protini yenye ubora wa hali ya juu kuliko kiasi kilichopo katika aina nyingine ya mazao ya mimea.ZK  taasisi inayojishughuliza na uzalishaji wa bidhaa za vyakula lishe na mimea na matunda, vinavyoweza kutiba magonjwa mbalimbali wamezalisha maziwa ya Soya ambayo yana  kiasi cha protini inayozidi hata kiasi cha protini katika nyama, mayai na maziwa. Hii inamaanisha kuwa maziwa ya soya ni chanzo rahisi na cha bei nafuu cha protini hasa kwa watu wenye kipato kidogo ambao hawawezi kumudu gharama za vyanzo vingine vya protini kama nyama, maziwa na samaki. Aidha, maziwa ya soya yanaa mafuta bora yasiyo kuwa na lehemu (cholesterol). Uwingi na ubora wa protini katika maziwa ya soya yanaweza kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto na kuwao...

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...