Skip to main content

UGONJWA WA BAWASIRI NA TIBA ZAKE

UJUE UGONJWA WA
(hemorrhoid) kuota kinyama sehemu ya haja kubwa.

Maada hii ni muhimu sana maana ni tatizo linalowatesa watu wengi ungana nami hapa uweze kupata elimu pia .
Bawasirini (kuota kinyama sehemu ya haja kubwa) ni uvimbe wa mishipa ya damu kwenye njia ya haja kubwa. Huonekana kutuna au kujaa kama jipu karibu na unyeo. Inaweza kutoa muwasho, hisia ya kuungua, au maumivu; hasa wakati wa kujisaidia. Wakati mwingine bawasiri hupasuka na kutoa damu kidogo nyekundu inayong’aa kwenye kinyesi.
Bawasiri ni tatizo la kawaida wakati wa ujauzito na miongoni mwa watu wanaokaa au kubeba mizigo mikubwa kutwa nzima, lakini kila mtu anaweza kuupata. Maumivu kutokana na bawasiri huzidi zaidi mgonjwa anapokuwa na tatizo la choo kigumu, kwa sababu kukitoa choo kigumu hulazimisha mishipa kwenye njia ya haja kubwa kupanuka zaidi.
bawasiri zipo za aina mbili.
1 Aina inayotembea (Yaani ikitoka ndani na kurudi)
2 Aina inayosimama

VISABABISHI VYA BAWASIRI (KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA)
Kisababishi kamili cha bawasiri hakijulikani. Baadhi ya vipengele vichangiapo ni pamoja na: Mazoea ya utumbo yasiyojirudia (kufungika kwa choo au kuhara), ukosefu wa mazoezi, visababishi vya lishe (chakula kilicho na kiwango cha chini cha faiba), ongezeko la shinikizo la ndani la fumbatio (uchovu unaoendelea kwa muda, asitisi, ukubwa wa ndani wa fumbatio, au ujauzito), jenetiki, kutokuwepo kwa vali katika vena ya hemoroidi, na kuongezeka kwa umri.
Visababishi vingine vinayoaminiwa kuongeza hatari ni pamoja na unene, kuketi chini kwa muda mrefu,[2] kikohozi kinachoendelea kwa muda na sakafu ya pelvisi kutofanya kazi.

JINSI YA KUEPUKANA NA HILI TATIZO LA BAWASIRI
•Epuka tatizo la ugumu wa choo na bawasiri kwa kujenga tabia ya kunywa maji mengi, kula matunda kwa wingi na nafaka nzimanzima ambazo hazijasindikwa.
•Baadhi ya juisi kutokana na mimea chungu ikipakwa kwenye bawasiri husaidia uvimbe kunywea.
•Kaa kwenye benseni au bafu yenye maji vuguvugu kusafisha bawasiri na kupunguza maumivu.   
•Usifute unyeo kwa kutumia mabunzi, gazeti, au vifaa vingine visivyo laini.
•Badala yake, tumia karatasi maalum ya kutawazia (toilet paper) au chombo cha maji kwa ajili ya kusafisha unyeo baada ya kujisaidia.

TIBA IFUATAYO HUSAIDIA KUPUNGUZA MAUMIVU NA KUONDOA BAWASIRI
UNAWEZA KUTUMIA KIMOJA WAPO
Kitunguu thaumu (Vijiko vitatu vya chakula), Asali (Nusu lita)
Tangawizi (Vijiko vitatu vya chakula)
MATUMIZI: Madawa haya lazima yapimwe kwa idadi hiyo yakiwa tayari yamekuwa unga, kisha changanya pamoja, na dozi yake ni kama ifuatayo; Kijiko kimoja cha unga wa madawa haya utakilamba asubuhi, mchana utafanya kama hivyo tena kisha jioni yaani (1 X 3) kwa muda wa siku saba hadi kumi na moja (7 - 11).
Natumai tumejifunza kitu ili kuweza kuepukana na tatizo Hili...
Na.. Elly Rodgers Masha..

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

Ndege ya Ukraine yaanguka Iran ikiwa na abiria 180, Abiria wote wafariki

Ndege ya Ukraine aina ya Boeing-737 iliyokuwa na abiria 180 imeanguka Iran, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo. Watoa huduma wa msalaba mwekundu wa Iran wanasema kuwa hakuna dalili yeyote kama kuna mtu aliyepona katika ajali hiyo. Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la kimataifa la ndege la Ukraine ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari katika uwanja wa ndege wa Imam Khomeini mjini Tehran. Ripoti za awali zinadai kuwa ndege hiyo ilikuwa safarini kuelekea mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.  Haijabainika ikiwa ajali hiyo ina uhusiano wowote na mzozo wa Iran-na Marekani. Kikosi cha uokoaji tayari kimetumwa katika eneo la tukio karibu na uwanja wa ndege, eneo ambalo ndege lilianguka. Credit: GettyImage " Ndege imeshika moto na tumetuma kikosi huko ... ," kiongozi wa huduma za dharura Pirhossein Koulivand,ameviambia vyombo vya habari ambapo Reuters imeripoti. Je tutegemee machafuko zaidi kutokea? Endelea kuwa pamoja nasi bega kwa bega, mshirikishe na mwenz...