Skip to main content

NAIBU SPIKA: WAPINZANI HAWAJUI KUZICHANGANUA HOJA LICHA YA UWASILISHAJI WAO MZURI



Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson.

Naibu spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt.  Tulia Ackson  amefunguka na kusema wabunge wa upinzani muda mwingine huwa wanaleta hoja nzuri kwa serikali lakini serikali inashindwa kuzipokea hoja hizo kutokana na uwasilishaji wao.

Naibu Spika amesema hayo leo Dodoma wakati akifanyiwa mahojiano katika kipindi cha bunge, ambapo alikuwa akitoa mtazamo wake juu ya bajeti kuu ya serikali kwa mwaka 2017/2018
"Wabunge wa upinzani muda mwingine wanaleta hoja nzuri sana bungeni lakini tatizo kubwa linakuja katika lugha inayotumika inakuwa si lugha ya staha ndiyo maana unaona hata serikali inakuwa haikubali. Bunge ni jumba la kisiasa, hivyo kila mwamba ngoma huvutia kwake, upande wa chama kinachoongoza ndiyo chenye serikali wana namna yao ya kuishauri serikali, ila wale ambao wanataka kuingia madarakani nao wana namna yao ya uchangiaji bungeni ndiyo maana kuna kuwa na mvutano wa hapa na pale" alisema  Tulia Ackson

Mbali na hilo Naibu Spika alidai serikali muda mwingine imekuwa inashindwa kufanyia kazi kwa haraka baadhi ya ushauri wa wabunge utolewao bungeni kutokana na ukweli kwamba serikali kabla ya kuleta jambo bungeni huwa inakuwa imefanya utafiti wa kutosha, hivyo linapoibuka jambo jipya inakuwa changamoto, inabidi ilichukue na kuja kulifanyia kazi siku za mbeleni.

Kuhusu upendeleo bungeni Naibu Spika amesema wabunge wote wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wapinzani wamekuwa wakipewa nafasi sawa lakini wabunge wa upinzani wamekuwa wakilalamika kutokana na kuwa na dhana ya kuonewa.

"Bunge hili limekuwa na wabunge zaidi ya 300 na walio wengi zaidi ni wabunge kutoka chama tawala, hivyo wale wa upinzani kwa kuwa wapo wachache hivyo wanaweza kuona kama wanaonewa hivi, wanaweza kuona kama hawasikilizwi, wanaona kama hawapewi muda zaidi, lakini unakuta mtu ukiwa kwenye kile kiti unawaza hili na kufanya utende kwa usawa tena kwa kuwasaidia walio wachache ili dhana hiyo isiwepo" alisisitiza Tulia Ackson

Kwa kumalizia  Tulia Ackson  aligusia jambo la mbunge kulishtaki bunge mahakamani na kusema kuwa hakuna mbunge anaweza kulishtaki bunge kama taasisi

"Bunge kama taasisi likifanya jambo huwezi kulipeleka mahakamani, bunge likiwa limefanya maamuzi juu ya jambo fulani na ukaona bunge halijafanya sawa kuna utaratibu wa kibunge lakini huwezi kuchukua maamuzi ya bunge ukapeleka mahakamani, kwa hiyo kuna utaratibu wake, lakini uamuzi wa bunge huwezi kuupeleka mahakamani kikanuni" alimalizia  Tulia Ackson

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

FAIDA ZA MAZIWA YA SOYA MWILINI

DONDOO ZA AFYA........!!!! MAAJABU YA SOYA MWILINI. MAAJABU YA SOYA MWILINI. Soya ni zao la jamii ya mikunde lenye aina nyingi za matumizi; ni zao linalofaa kwa chakula cha binadamu na wanyama na pia ni zao la biashara. Zao hilo lina kiasi kingi cha protini yenye ubora wa hali ya juu kuliko kiasi kilichopo katika aina nyingine ya mazao ya mimea.ZK  taasisi inayojishughuliza na uzalishaji wa bidhaa za vyakula lishe na mimea na matunda, vinavyoweza kutiba magonjwa mbalimbali wamezalisha maziwa ya Soya ambayo yana  kiasi cha protini inayozidi hata kiasi cha protini katika nyama, mayai na maziwa. Hii inamaanisha kuwa maziwa ya soya ni chanzo rahisi na cha bei nafuu cha protini hasa kwa watu wenye kipato kidogo ambao hawawezi kumudu gharama za vyanzo vingine vya protini kama nyama, maziwa na samaki. Aidha, maziwa ya soya yanaa mafuta bora yasiyo kuwa na lehemu (cholesterol). Uwingi na ubora wa protini katika maziwa ya soya yanaweza kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto na kuwao...

Supplements During Pregnancy: What’s Safe and What’s Not

AUTHORITY NUTRITION Evidence Based Supplements During Pregnancy: What’s Safe and What’s Not Pregnancy can be one of the most exciting and happy experiences in a woman’s life. However, it can also be a confusing and overwhelming time for some mothers-to-be. The internet, magazines and advertisements flood women with advice on how to stay healthy during pregnancy. While most women know that high-mercury seafood, alcohol and cigarettes are off-limits during pregnancy, many are unaware that some vitamins, minerals and herbal supplements should be avoided as well. Information on which supplements are safe and which aren’t often varies between sources, making things more complicated. This article breaks down which supplements are believed to be safe to take during pregnancy and explains why some supplements must be avoided. Why Take Supplements During Pregnancy? Consuming the right nutrients is important at every stage of life, but it’s especially crit...