Skip to main content

MAWAKILI MTAJIFICHA WAPI? OFISI ZA PRIME ATTONEY ZAVAMIWA

Wiki mbili baada ya ofisi za mawakili ya Prime Attorneys jijini Dar es Salaam kuvamiwa usiku wa manane na watu wasiojulikana, ofisi nyingine ya mawakili imefanyiwa uhalifu wa aina hiyo mjini hapa.

Katika uvamizi wa ofisi za mawakili za Prime Attoneys ambao pia wanamteta mfanyabiashara maarufu Yusuf Manji, wezi waliiba sefu ya fedha na nyaraka baada ya kumfunga kamba mlinzi.

Mmoja wa mawakili wa kampuni hiyo, Hudson Ndusyepo alisema katika uvamizi wa ofisi hizo zilizopo kwenye jengo la Prime House, Mtaa wa Tambaza, Upanga nyaraka za mfanyabiashara huyo hazikuibwa.

Wakati uvamizi wa ofisi hizo ukiacha utata, watu wasiojulikana walivunja na kuiba mali mbalimbali katika ofisi mbili za mawakili jijini Arusha tukio ambalo limeibua hali ya hofu na sintofahamu kwa baadhi ya mawakili.

Ofisi zilizovamiwa ni za Ideal Chambers iliyopo jengo la Blue Rock na Equality Attorneys yenye maskani yake katika jengo la Said Kondo zote zikiwa katikati ya jiji.

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo alithibitisha kwa kifupi kuvamiwa kwa ofisi hizo akisema polisi wanaendelea na uchunguzi wa matukio hayo.

Wakili Edmund Mgemela wa kampuni ya Equality Attornerys alielezea kuwa tukio hilo lilitokea mwezi uliopita ambapo mara baada ya kuwasili asubuhi alikuta mlango wa ofisi ukiwa wazi na umevunjwa.

Mgemela alisema baada ya kuingia ndani alikuta baadhi ya nyaya za kompyuta ofisini zimenyofolewa, baadhi ya nyaraka zimechukuliwa sanjari na suti ambazo huzihifadhi ofisini kwake pia hazikuzikuta.

Hatahivyo, alisema kwamba aliripoti tukio hilo polisi na kupewa RB namba 790/2017 akiamini wahusika walikuwa na nia ovu kwa kuwa ndani ya jengo analofanyia shughuli zake kuna ofisi mbalimbali ambazo hazikuguswa siku ya tukio. “Mpaka sasa sielewi kama ni visasi au la, lakini ninachoweza kusema ni kwamba hawa watu walikuwa na nia ovu haiwezekani ndani ya jengo hili kuna ofisi nyingi wazipite zote kuanzia ghorofa ya kwanza mpaka wafike ya tatu kwangu na kuvunja,” alisema Mgemela.

Wakili kutoka Ideal Chambers, Robert Akileti alisema uvamizi katika ofisi yao ulifanywa Agosti 10 ambapo watu hao walivunja mchana alipokuwa ameenda kupata mlo.

Akileti alisema kuwa aliporejea ofisini kuendelea na shughuli zake alikuta mlango wa ofisi umevunjwa na kompyuta tatu mpakato (laptop)zimeibiwa kitendo ambacho kiliwapa hofu na mpaka sasa hawaelewi watu hao walikuwa na nia gani.
 
Kwa habari habari nyingine bofya hapa

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

Ndege ya Ukraine yaanguka Iran ikiwa na abiria 180, Abiria wote wafariki

Ndege ya Ukraine aina ya Boeing-737 iliyokuwa na abiria 180 imeanguka Iran, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo. Watoa huduma wa msalaba mwekundu wa Iran wanasema kuwa hakuna dalili yeyote kama kuna mtu aliyepona katika ajali hiyo. Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la kimataifa la ndege la Ukraine ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari katika uwanja wa ndege wa Imam Khomeini mjini Tehran. Ripoti za awali zinadai kuwa ndege hiyo ilikuwa safarini kuelekea mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.  Haijabainika ikiwa ajali hiyo ina uhusiano wowote na mzozo wa Iran-na Marekani. Kikosi cha uokoaji tayari kimetumwa katika eneo la tukio karibu na uwanja wa ndege, eneo ambalo ndege lilianguka. Credit: GettyImage " Ndege imeshika moto na tumetuma kikosi huko ... ," kiongozi wa huduma za dharura Pirhossein Koulivand,ameviambia vyombo vya habari ambapo Reuters imeripoti. Je tutegemee machafuko zaidi kutokea? Endelea kuwa pamoja nasi bega kwa bega, mshirikishe na mwenz...