Skip to main content

MAWAKILI MTAJIFICHA WAPI? OFISI ZA PRIME ATTONEY ZAVAMIWA

Wiki mbili baada ya ofisi za mawakili ya Prime Attorneys jijini Dar es Salaam kuvamiwa usiku wa manane na watu wasiojulikana, ofisi nyingine ya mawakili imefanyiwa uhalifu wa aina hiyo mjini hapa.

Katika uvamizi wa ofisi za mawakili za Prime Attoneys ambao pia wanamteta mfanyabiashara maarufu Yusuf Manji, wezi waliiba sefu ya fedha na nyaraka baada ya kumfunga kamba mlinzi.

Mmoja wa mawakili wa kampuni hiyo, Hudson Ndusyepo alisema katika uvamizi wa ofisi hizo zilizopo kwenye jengo la Prime House, Mtaa wa Tambaza, Upanga nyaraka za mfanyabiashara huyo hazikuibwa.

Wakati uvamizi wa ofisi hizo ukiacha utata, watu wasiojulikana walivunja na kuiba mali mbalimbali katika ofisi mbili za mawakili jijini Arusha tukio ambalo limeibua hali ya hofu na sintofahamu kwa baadhi ya mawakili.

Ofisi zilizovamiwa ni za Ideal Chambers iliyopo jengo la Blue Rock na Equality Attorneys yenye maskani yake katika jengo la Said Kondo zote zikiwa katikati ya jiji.

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo alithibitisha kwa kifupi kuvamiwa kwa ofisi hizo akisema polisi wanaendelea na uchunguzi wa matukio hayo.

Wakili Edmund Mgemela wa kampuni ya Equality Attornerys alielezea kuwa tukio hilo lilitokea mwezi uliopita ambapo mara baada ya kuwasili asubuhi alikuta mlango wa ofisi ukiwa wazi na umevunjwa.

Mgemela alisema baada ya kuingia ndani alikuta baadhi ya nyaya za kompyuta ofisini zimenyofolewa, baadhi ya nyaraka zimechukuliwa sanjari na suti ambazo huzihifadhi ofisini kwake pia hazikuzikuta.

Hatahivyo, alisema kwamba aliripoti tukio hilo polisi na kupewa RB namba 790/2017 akiamini wahusika walikuwa na nia ovu kwa kuwa ndani ya jengo analofanyia shughuli zake kuna ofisi mbalimbali ambazo hazikuguswa siku ya tukio. “Mpaka sasa sielewi kama ni visasi au la, lakini ninachoweza kusema ni kwamba hawa watu walikuwa na nia ovu haiwezekani ndani ya jengo hili kuna ofisi nyingi wazipite zote kuanzia ghorofa ya kwanza mpaka wafike ya tatu kwangu na kuvunja,” alisema Mgemela.

Wakili kutoka Ideal Chambers, Robert Akileti alisema uvamizi katika ofisi yao ulifanywa Agosti 10 ambapo watu hao walivunja mchana alipokuwa ameenda kupata mlo.

Akileti alisema kuwa aliporejea ofisini kuendelea na shughuli zake alikuta mlango wa ofisi umevunjwa na kompyuta tatu mpakato (laptop)zimeibiwa kitendo ambacho kiliwapa hofu na mpaka sasa hawaelewi watu hao walikuwa na nia gani.
 
Kwa habari habari nyingine bofya hapa

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA ASILI NA USAFI KWA WANAWAKE NI MUHIMU

Dawa ya Uchafu Ukeni Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano. Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’. Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla. Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni: • Kuwa na wapenzi wengi • Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango • Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali • Uchafu • Uvutaji sigara • Pombe • Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni Dalili: • Kutokwa na uchafu us...

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

FAIDA ZA MAZIWA YA SOYA MWILINI

DONDOO ZA AFYA........!!!! MAAJABU YA SOYA MWILINI. MAAJABU YA SOYA MWILINI. Soya ni zao la jamii ya mikunde lenye aina nyingi za matumizi; ni zao linalofaa kwa chakula cha binadamu na wanyama na pia ni zao la biashara. Zao hilo lina kiasi kingi cha protini yenye ubora wa hali ya juu kuliko kiasi kilichopo katika aina nyingine ya mazao ya mimea.ZK  taasisi inayojishughuliza na uzalishaji wa bidhaa za vyakula lishe na mimea na matunda, vinavyoweza kutiba magonjwa mbalimbali wamezalisha maziwa ya Soya ambayo yana  kiasi cha protini inayozidi hata kiasi cha protini katika nyama, mayai na maziwa. Hii inamaanisha kuwa maziwa ya soya ni chanzo rahisi na cha bei nafuu cha protini hasa kwa watu wenye kipato kidogo ambao hawawezi kumudu gharama za vyanzo vingine vya protini kama nyama, maziwa na samaki. Aidha, maziwa ya soya yanaa mafuta bora yasiyo kuwa na lehemu (cholesterol). Uwingi na ubora wa protini katika maziwa ya soya yanaweza kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto na kuwao...