Skip to main content

DK. HASSAN ABBAS- UCHUMI WA NCHI UKO IMARA SANA

YALIYOSEMWA NA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI DK. HASSAN ABBAS JUU YA HALI YA UCHUMI WA NCHI ULIVYO SASA

“Uchumi wa Tanzania kwa miaka mitatu mfululizo sasa bado uko katika ukuaji usiopungua asilimia 7.0 hadi 7.2 ikiwa ni ukuaji wa juu katika ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Rwanda inakua kwa asilimia 6, Uganda asilimia 5 na Kenya asilimia 6.4” -  Dkt. Abbasi.

"Sambamba na ukuaji wa uchumi, Tanzania imeendelea kudhibiti mfumuko wa bei ambapo taarifa ya hivi karibuni zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonesha kuwa mfumuko wa bei nchini umeshuka kutoka asilimia 6.1 mwezi Mei hadi kufikia asilimia 5.4 mwezi Juni mwaka huu" - Dk. Abbas

"Takwimu za taasisi ya Quantum Global Research Lab ya Uingereza imeeleza Farihisi ya Uwekezaji Afrika ambazo zilionesha Tanzania ikiongoza miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki na ya nane Barani Afrika, ikiwa imepanda kutoka nafasi ya 19 mwaka 2015" - Dk. Abbas

“Mashirika ya Kimataifa kama IMF, Benki ya Dunia katika ripoti zao za hivi karibuni yamesisitiza kuwa uchumi wa Tanzania ni imara na wamesifu mageuzi makubwa yanayofanywa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli”- Dkt. Abbasi

"Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kufanyia kazi maoni hayo ya IMF na Benki ya Dunia na kwamba mabadiliko makubwa yamefanyika katika kupambana na rushwa na kudhibiti mapato ya Serikali ambapo ukusanyaji wa mapato umeongezeka kutoka wastani wa shilingi bilioni 925 kwa mwaka 2015 hadi shilingi trilioni 1.069 kwa mwaka 2016/17 ikiwa ni ongezeko la asilimia 15" - Dk. Abbas

"Kutokana na uchumi wa Tanzania kuwa imara kumeiwezesha Serikali kufanya maboresho makubwa katika sekta mbalimali zikiwemo afya, elimu, miundombinu na nishati ambapo katika sekta ya afya Serikali imetenga shilingi trilioni 1.077 kwa mwaka wa fedha 2017/18 kulinganisha na shilingi bilioni 796 zilizotengwa mwaka fedha 2016/17" - Dk. Abbas

"Upande dawa na vifaa tiba, Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kutekeleza ahadi yake kwa kuongeza fedha katika ununuzi wa dawa ambapo katika kipindi cha miaka mitatu fedha za ununuzi wa dawa na vifaa tiba zimeongezea kutoaka shilingi bilioni 30 mwaka 2015/16 mpaka kufikia shilingi bilioni 261 katika bajeti ya mwaka 2017/18" - Dk. Abbas

“Katika kuhakikisha Watanzania wengi wanaelimika, Serikali imeendelea kutoa elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne ambapo takribani shilingi bilioni 18 hutumika kwa mwezi na zinawafikia walengwa na kwa wakati” - Dkt. Abbasi 

"Wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani kulikuwa na shilingi bilioni 341 kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu lakini Rais John Pombe Magufuli akaongeza hadi kufikia shilingi bilioni 475 na kwa mwaka 2016/17 bajeti ya mikopo ya elimu juu iliongezeka hadi kufikia shilingi bilioni 483" - Dk. Abbas

"Kutokana na uchumi imara, Tanzania imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali mikubwa ya maendeleo ikiwemo ile ya umeme, maji, reli ya kisasa, barabara na pia mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda mapka Tanga nchini Tanzania, ambapo mradi huu unatekelezwa kwa pamoja na nchi hizo mbili" - Dk. Abbas

Comments

Popular posts from this blog

DAWA YA ASILI NA USAFI KWA WANAWAKE NI MUHIMU

Dawa ya Uchafu Ukeni Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano. Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’. Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla. Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni: • Kuwa na wapenzi wengi • Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango • Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali • Uchafu • Uvutaji sigara • Pombe • Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni Dalili: • Kutokwa na uchafu us...

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

FAIDA ZA MAZIWA YA SOYA MWILINI

DONDOO ZA AFYA........!!!! MAAJABU YA SOYA MWILINI. MAAJABU YA SOYA MWILINI. Soya ni zao la jamii ya mikunde lenye aina nyingi za matumizi; ni zao linalofaa kwa chakula cha binadamu na wanyama na pia ni zao la biashara. Zao hilo lina kiasi kingi cha protini yenye ubora wa hali ya juu kuliko kiasi kilichopo katika aina nyingine ya mazao ya mimea.ZK  taasisi inayojishughuliza na uzalishaji wa bidhaa za vyakula lishe na mimea na matunda, vinavyoweza kutiba magonjwa mbalimbali wamezalisha maziwa ya Soya ambayo yana  kiasi cha protini inayozidi hata kiasi cha protini katika nyama, mayai na maziwa. Hii inamaanisha kuwa maziwa ya soya ni chanzo rahisi na cha bei nafuu cha protini hasa kwa watu wenye kipato kidogo ambao hawawezi kumudu gharama za vyanzo vingine vya protini kama nyama, maziwa na samaki. Aidha, maziwa ya soya yanaa mafuta bora yasiyo kuwa na lehemu (cholesterol). Uwingi na ubora wa protini katika maziwa ya soya yanaweza kuondoa utapiamlo hususani kwa watoto na kuwao...