Skip to main content

JE WAIFAHAMU HOMA YA INI NA MADHARA YAKE

*HEPATITIS(Homa ya ini)*

Hepatitis B ni maambukizi mabaya sana ya kirusi aitwaye hepatitis B virus (HBV) kwenye  maini. Kwa watu wengine ugonjwa huu huweza kuchukua zaidi ya miezi 6 (chronic). Ugonjwa huu ukichukua muda mrefu unaweza kuleta madhara ya kufeli kwa ini, kansa ya ini au liver cirrhosis hali ambayo itaacha makovu ya kudumu kwenye maini. Watu wengi wanaougua ugonjwa huu hupona kabisa.
Kuna chanjo ya kusaidia kuzuia hepatitis B lakini hakuna tiba pale ambapo tayari utakuwa umeambukizwa virusi wa hepatitis B. Ukishaambukizwa yafaa kuchukua tahadhari za kusaidia kutowaambukiza watu wengine.

*Dalili Za Hepatitis B*

Dalili za hepatitis B huanza kuonekana baada ya mwezi mmoja hadi minne baada ya kupata maambukizi, nazo ni:
. Maumivu ya tumbo
. Mkojo mweusi
. Homa
. Maumivu ya joints
. Kukosa hamu ya kula
. Kichefuchefu na kutapika
. Udhaifu wa mwili na mwili kukosa nguvu
. Macho na ngozi kugeuka rangi na kuwa vya njano

*Chanzo Cha Hepatitis B*
Ugomjwa wa hepatitis B husababishwa na kirusi aitwaye Hepatitis B virus (HBV). Kirusi huyu huambukizwa kutoka mtu mmoja hadi mwingine kupitia damu, shahawa na maji maji mengine ya mwilini.

Njia kuu za uambukizaji zikiwa:
. Kujamiiana. Unaweza kuambukizwa na mtu mwenye ugonjwa huo kama utajamiiana naye bila kutumia kinga na damu, mate, shahawa au maji maji ya ukeni yakaingia ndani ya mwili wako.
. Kuchangia sindano. Kirusi wa hepatitis B anaambukiza kirahisi sana kupitia sindano zenye damu ya mtu mwenye virusi hivi.
. Mama kumwambukiza mtoto. Mama mwenye mimba mwenye virusi vya HBV anaweza kumwambukiza kichanga wakati wa tendo la uzazi. Mtoto anaweza kupewa chanjo baada ya kuzaliwa na akaepuka kuambukizwa, hivyo ni vizuri kuchukua tahadhari ya kujipima wakati una ujauzito.

Hepatitis B hugawanywa katika makundi mawili; Hepatitis ya muda mfupi (acute hepatitis) na hepatitis ya muda mrefu (chronic hepatitis).

Acute hepatitis B: Hii huchukua chini ya miezi 6 kupona. Kinga zako za mwili zinaweza kupambana na kuuondoa ugonjwa huu na ukapona kabisa katika muda mfupi. Watu wazima mara nyingi huugua acute hepatitis ingawa mara chache huweza kufikia kuwa chronic hepatitis.

Chronic hepatitis B: Ugonjwa huu huchukua miezi 6 au zaidi kupona. Kama kinga za mwili wako hazitaweza kuushinda, basi ugonjwa utakuwa ni wa maisha kwako na uwezekano wa maganjwa makubwa zaidi kama ya cirrhosis na saratani ya ini ukiongezeka. Chronic hepatitis B inaweza isigundulike kwa miaka mingi hadi mgonjwa atakapokuwa mahututi kutokana na ugonjwa huu wa homa ya ini.

*Madhara ya hepatitis B*
Kuwa na hepatitis B kwa muda mrefu (chronic hepatits) kunaweza kusababisha madhara makubwa yafutayo;
. Makovu kwenye ini (Cirrhosis). Kuvimba kwa ini kwa muda mrefu kunakotokana na virusi wa hepatitis B kunaweza kusababaisha makovu kwenye ini (cirrhosis) na kulifanya ini lishindwe kufanya kazi yake inavyotakiwa.
. Saratani ya ini. Watu wenye hapatitis B kwa muda mrefu wanaweza baadaye wakapata saratani ya ini.
. Ini kufeli. Ini likishindwa kufanya kazi zake kabisa, hatua nyingine ya kuwekewa ini jingine itahitajika.
. Matatizo mengine. Mgonjwa mwenye hepatitis B anaweza kupata matatizo ya figo, uvimbe kwenye mishipa ya damu na upungufu wa damu.
Tiba Ya Hepatitis B
Kama vipimo vikionyesha kuwa una hepatitis B ya muda mfupi (acute hepatitis), huhitaji tiba kwa sababu itaondoka yenyewe baada ya muda mfupi. Badala yake unahitaji kupumzika, kupata lishe bora na vinywaji vya kutosha wakati kinga zako za mwili zikipambana kuundoa ugonjwa huo.

*Dawa ya kutibu homa ya ini*

yaani zaidi ya miezi sita, utahitaj tiba ili kuondoa madhara ya ugonjwa huo na kuzuia usiwaambukize watu wengine.

Baadhiya tiba ni:
. Dawa za kuua virusi (antiviral medications) . Kuna dawa nyingi za kuweza kuua virusi ikiwa ni pamoja na lamivudine (Epivir), adefovir (Hepsera), telbivudine (Tyzeka) na entecavir (Baraclude).
. Interferon alfa-2b (Intron A). Hii hutolewa kama sindano na hasa hutumika kwa vijana wadogo au wanaotegemea kupata ujauzito. Madhara ya tiba hii ni kupata mfadhaiko, kubanwa kifua na kupumua kwa shida.
. Kubadilishiwa Maini. Kama maini yako yameharibika kabisa, upasuaji hufanyika na kuwekewa maini mengine.
   *xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx*

*Dr. Brown Fm*

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

Ndege ya Ukraine yaanguka Iran ikiwa na abiria 180, Abiria wote wafariki

Ndege ya Ukraine aina ya Boeing-737 iliyokuwa na abiria 180 imeanguka Iran, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo. Watoa huduma wa msalaba mwekundu wa Iran wanasema kuwa hakuna dalili yeyote kama kuna mtu aliyepona katika ajali hiyo. Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la kimataifa la ndege la Ukraine ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari katika uwanja wa ndege wa Imam Khomeini mjini Tehran. Ripoti za awali zinadai kuwa ndege hiyo ilikuwa safarini kuelekea mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.  Haijabainika ikiwa ajali hiyo ina uhusiano wowote na mzozo wa Iran-na Marekani. Kikosi cha uokoaji tayari kimetumwa katika eneo la tukio karibu na uwanja wa ndege, eneo ambalo ndege lilianguka. Credit: GettyImage " Ndege imeshika moto na tumetuma kikosi huko ... ," kiongozi wa huduma za dharura Pirhossein Koulivand,ameviambia vyombo vya habari ambapo Reuters imeripoti. Je tutegemee machafuko zaidi kutokea? Endelea kuwa pamoja nasi bega kwa bega, mshirikishe na mwenz...