Skip to main content

TIBA ZA ASILI KWA KIKOHOZI

🌸🌻AJINSI YA KUTIBU KIKOHOZI KWA NJIA ZA ASILI.
Kama umekuwa ni miomgoni mwa watu ambao wamekuwa wakisumbuliwa na kikohozi kwa muda mrefu anaweza kutumia vitu vifuaravyo ili uweze kupona kabisa,

1. Tangawizi
Tangawizi ni moja ya dawa maarufu kwa kutibu kikohozi.
Tengeneza chai ukitumia tangawizi mbichi na ndani yake utumie asali na siyo sukari kwenye hii chai yako. Kunywa kikombe kimoja kutwa mara 3 kila siku mpaka umepona.
Angalizo usitumie dawa hii kama una ujauzito mchanga chini ya miezi minne na hata ukiwa na ujauzito zaidi ya miezi minne basi tumia kikombe kimoja tu kwa siku.
Unaweza pia kutengeneza juisi ya tangawizi freshi ukiongeza parachichi ndani yake na unywe kwa mtindo huo huo wa chai hapo juu.

2. Limau
Limau inaweza kutumika kwa namna nyingi katika kutibu kikohozi. Limau zina sifa za kuondoa maambukizi na pia limau lina vitamini mhimu ambayo hupigana na maambukizi na kukuongezea kinga ya mwili vitamini mhimu sana vitamini C.

Changanya vijiko vikubwa viwili vya maji maji ya limau na kijiko kikubwa kimoja cha asali mbichi na unywe mchanganyiko huu mara 2 kwa siku kwa siku kadhaa.

3. Kitunguu swaumu
Kitunguu swaumu kina sifa ya kuua bakteria na virusi mwilini sifa ambayo inakifanya kuwa dawa bora ya kutibu kikohozi.

Menya punje 6 za kitunguu swaumu, kata vipande vidogo vidogo (chop) na uchanganye kwenye kikombe kimoja (robo lita) cha asali na uuache mchanganyiko huu kwa usiku mzima.
Kuanzia kesho yake asubuhi chukua kijiko kidogo kimoja cha mchanganyiko huu na ulambe mara 2 kwa siku mpaka upone.
 

4. Kitunguu maji
Moja ya dawa nyingine rahisi ya kutibu kikohozi ni kitunguu maji. Unaweza kunusa tu mara kadhaa harufu ya kitunguu na ukaona mabadiliko.

Changanya kijiko kidogo kimoja cha juisi ya kitunguu maji na kijiko kidogo kimoja cha asali mbichi na unywe mara 2 kwa siku mchanganyiko huu kwa siku kadhaa.
 

5. Maziwa ya moto na asali.
Maziwa ya moto na asali vinaweza kusaidia kutibu kikohozi kikavu na kupunguza maumivu ya kifua ambayo hutokeo kama matokeo ya kukohoa mfululizo kwa kipindi kirefu.

Kwa matokeo mazuri kunywa dawa hii kabla ya kwenda kulala. Changanya kijiko kikubwa kimoja cha asali mbichi ndani ya nusu kikombe (ml 125) cha maziwa ya moto na unywe kabla ya kwenda kulala kila siku, Hii itasaidia kusafisha na kulainisha koo lako haraka.

6. Zabibu
Zabibu zinazo kazi na sifa kuu ya kuondoa makohozi na uchafu mwingine kwenye mfumo wako wa upumuwaji wa mwili. Kadri unavyoondoa haya makohozi kwenye mfumo wako ndivyo unavyopona kwa haraka kikohozi.

Unaweza kula tu zabibu kadhaa kila siku au tengeneza juisi freshi ya zabibu na unywe kikombe kimoja kutwa mara 2 kwa siku kadhaa mpaka umepona.

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

Ndege ya Ukraine yaanguka Iran ikiwa na abiria 180, Abiria wote wafariki

Ndege ya Ukraine aina ya Boeing-737 iliyokuwa na abiria 180 imeanguka Iran, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo. Watoa huduma wa msalaba mwekundu wa Iran wanasema kuwa hakuna dalili yeyote kama kuna mtu aliyepona katika ajali hiyo. Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la kimataifa la ndege la Ukraine ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari katika uwanja wa ndege wa Imam Khomeini mjini Tehran. Ripoti za awali zinadai kuwa ndege hiyo ilikuwa safarini kuelekea mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.  Haijabainika ikiwa ajali hiyo ina uhusiano wowote na mzozo wa Iran-na Marekani. Kikosi cha uokoaji tayari kimetumwa katika eneo la tukio karibu na uwanja wa ndege, eneo ambalo ndege lilianguka. Credit: GettyImage " Ndege imeshika moto na tumetuma kikosi huko ... ," kiongozi wa huduma za dharura Pirhossein Koulivand,ameviambia vyombo vya habari ambapo Reuters imeripoti. Je tutegemee machafuko zaidi kutokea? Endelea kuwa pamoja nasi bega kwa bega, mshirikishe na mwenz...