Skip to main content

Lijue tatizo la Ugumba kwa akina mama

Ugumba wa mwanamke unasababishwa na nini?

Ugumba wa mwanamke ni hali ya mwanamke kushindwa kupata mimba. Kama kwa wanaume kuna mambo mengi yanayoweza kusababisha ugumba wa wanawake.
Ili mwanamke aweze kupata mimba, vitu vingi lazima vitokee. Lazima yai lipevushwe, lazima yai lii ngie kwenye mrija wa kupitisha yai ambapo mimba hutungwa, tena lazima yai lililorutubishwa lifikie kwenye mfuko wa mimba na mwishoni lazima utando ndani ya mfuko wa uzazi uandaliwe. Endapo yoyote kati ya hali hizi hazitafikiwa kwa sababu fulani, mimba haiwezi kutunga. Sababu za kutopevuka yai mara nyingi ni mfadhaiko wa kiakili na kisaikologia na sababu za kuziba mrija wa kupitisha yai mara nyingi ni magonjwa ya zinaa. Wanawake wengine wamepata ugumba kutokana na kujaribu kutoa mimba, matokeo yake wameziharibu kabisa sehemu za ndani za viungo vya uzazi. Bahati mbaya, hali nyingi katika hizi haziwezi kurekebishwa na wanawake wanabaki wagumba wa kudumu.
Kuna mambo mengine yanayosababisha ugumba wa muda. Mambo hayo ni pamoja na ugonjwa, ulevi, matumizi ya dawa za kulevya, lishe duni, mshituko na majonzi. Vingi vya vyanzo hivi vinaweza kutibwa, kwa mfano, kutumia madawa ya kulevya. Mara vikitibiwa, mwanamke ataweza kupata mimba.

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

Ndege ya Ukraine yaanguka Iran ikiwa na abiria 180, Abiria wote wafariki

Ndege ya Ukraine aina ya Boeing-737 iliyokuwa na abiria 180 imeanguka Iran, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo. Watoa huduma wa msalaba mwekundu wa Iran wanasema kuwa hakuna dalili yeyote kama kuna mtu aliyepona katika ajali hiyo. Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la kimataifa la ndege la Ukraine ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari katika uwanja wa ndege wa Imam Khomeini mjini Tehran. Ripoti za awali zinadai kuwa ndege hiyo ilikuwa safarini kuelekea mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.  Haijabainika ikiwa ajali hiyo ina uhusiano wowote na mzozo wa Iran-na Marekani. Kikosi cha uokoaji tayari kimetumwa katika eneo la tukio karibu na uwanja wa ndege, eneo ambalo ndege lilianguka. Credit: GettyImage " Ndege imeshika moto na tumetuma kikosi huko ... ," kiongozi wa huduma za dharura Pirhossein Koulivand,ameviambia vyombo vya habari ambapo Reuters imeripoti. Je tutegemee machafuko zaidi kutokea? Endelea kuwa pamoja nasi bega kwa bega, mshirikishe na mwenz...