Skip to main content

JE WAJUA KUWA TENDO LA NDOA NI TIBA NA DAWA KIAFYA?

❤FAIDA 15 ZA KUSHIRIKI TENDO LA NDOA❤

Tendo la ndoa tangu uumbaji lililengwa kati ya mwanaume na mwanamke waliofunga ndoa,
sasa hivi dunia imebadilika sana kiasi kwamba tendo hili sio lazima kuliita la ndoa tena. watu wengi wamekua wakishiriki tendo la ndoa bila kufungua ndoa .. vile vile kutokujua faida zake.lakini tendo la ndoa lina faida nyingi sana kiafya na kisaikolojia.
Hivyo kama wewe una mke, mchumba au mpenzi halafu kila siku unampa sababu za kutoshiriki basi huenda hujui faida zake. hebu tuzisome kama ifuatavyo..

👉🏿 HUONDOA MSONGO WA MAWAZO;
    kipindi cha tendo la ndoa mwili hutoa hormone inayoitwa kitaalamu kama endophirn ambayo huleta furaha.kila aliyeshiriki tendo la ndoa atakua shahidi kama una msongo wa mawazo sana ukaenda kufanya tendo hili utajikuta unajisikia vizuri sana,

👉🏿 HUPUNGUZA PRESHA YA DAMU;
     wakati wa tendo la ndoa damu inapita kwa kasi sana kwenye mishipa ya damu na kuondoa vikwazo kama mafuta, lehemu na kunyoosha mishipa iliyosinyaa.utafiti unaonyesha tendo la ndo hushusha presha ya chini kitaalamu kama diastolic pressure.

👉🏿 HUONGEZA KINGA YA MWILI;
    askari wa mwili kwa jina immunoglubin hutolewa na mwili kupambana na magonjwa wakati wa tendo la ndoa, kama huamini basi shiriki tendo la ndoa ukiwa na mafua na baadae utashindwa kuelewa mafua yameenda wapi.

👉🏿 HUIMARISHA MAHUSIANO;
      kuna homoni ya furaha na uzazi inaitwa oxytocin homoni, homoni hii hutengenezwa na mwili kipind cha tendo la ndoa.kama umekaa kwenye mahuasiano muda mrefu utagundua kwamba ikitokea umegombana na mpenzi wako halafu mkafanya tendo la ndoa basi ugomvi unaisha bila hata kuongelea swala lililowagombanisha.

👉🏿 HUPUNGUZA UWEZEKANO WA KUPATA KANSA YA TEZI DUME;
    utafiti uliofanyika nchini australia uligundua kwamba wanaume wanaoshiriki tendo la ndoa angalaua mara 21 kwa mwezi wako kwenye hatari ndogo sana ya kupata kansa ya tezi dume kuliko wale wasioshiriki hivyo kama mpenzi au mke wako hakupi ushirikiano basi atakuletea kansa.

👉🏿 HUSAIDIA KUPATA HEDHI KWA WAKATI;
    tendo la ndoa huweka homone za uzazi kitaalamu kama oestrogen na progesterone kwenye kiwango sawa. hii husaidia kupata siku zako kwa wakati na bila maumivu.kimsingi tendo la ndoa husaidia sana kuliko vidonge vya uzazi ambavyo humezwa na watu ambao hawaoni siku zao.

👉🏿 HULETA USINGIZI WA KUTOSHA;
     hii haihitaji ubishi au ushahidi mara nyingi baada ya kushiriki tendo la ndoa hata kama ni mchana kila mtu hupata uchovu fulani na kujikuta unapitiwa na usingizi kwa muda mrefu.

👉🏿 NISEHEMU YA MAZOEZI;
   tendo la ndoa lina faida zote ambazo mtu anayefanya mazoezi anazipata ikiwemo kupungua uzito, kua na afya bora hata kuondoa kitambi kwani wakati wa tendo la ndoa mapigo ya moyo huongezeka, kasi ya upumuaji hua juu na kua sawa na mtu wa mazoezi.

👉🏿 HUKUFANYA UISHI MUDA MREFU;
    moja ya sababu kuu zinazofanya watu wafe mapema ni kukosa furaha ya maisha, na kua na afya ambayo sio nzuri.watu wanaoshiriki tendo la ndoa wanapata faida za kua na afya bora na furaha.

👉🏿 HUONGEZA NGUVU ZA KIUME NA UWEZO WA KUFANYA TENDO;
     watu wengi wenye umri zaidi ya miaka 40 huanza kupungukiwa nguvu za kiume. hii ni sababu ya damu kidogo ambayo inafika kwenye uume. tendo la ndoa mara kwa mara hupeleka damu nyingi kwenye uume na kukufanya ue na uume imara na wenye nguvu.

👉🏿 HUKIFANYA UONEKANE MDOGO KIUMRI;
    tendo la ndoa mara kwa mara hukufanya mwili uwe bize kumwaga homoni mbalimbali mwilini ambazo humfanya mtu aonekane mdogo kwa miaka kumi ukilinganisha na umri wake halisi.

👉🏿 HUIMARISHA AFYA YA MOYO;
    tendo la ndoa huchoma mafuta ambayo ni sumu kwa moyo, mafuta mengi huweza kuziba mishipa ya moyo na kusababisha shambulio la moyo kitaalamu kama heart attack.

👉🏿 HUONGEZA NGUVU KWENYE MISULI YA NYONGA;
     katika umri fulani mkubwa wanawake hupata matatizo ya kushindwa kuzuia mkojo sababu ya kuzaa mara kwa mara. kipindi cha tendo la ndoa wakati mwanamke anafika kileleni uke wake unabana sana na kufanya misuli yake ya nyonga kua na nguvu.

👉🏿 HUPUNGUZA MAUMIVU;
     utafiti uliofanywa na madaktari bingwa wa mifupa umegundua kwamba wagonjwa wa baridi yabisi au athritis ambao wanashiriki tendo la ndoa mara kwa mara hawasumbuliwi sana na maumivu kama hao wasio shiriki.

MWISHO; wanawake wengi sana walioko kwenye mahusiano au waliolewa hua ni wanakua na sababu nyingi sana za kutoshiriki tendo la ndoa. hii ni moja ya vyanzo vikuu vya wanaume kutoka nje ya ndoa kwani kitaalamu mwanume muda wote ana hamu ya kushiriki tendo la ndoa sasa unapo muwekea vikwazo basi kwenda nje ni lazima.sasa kabla hujaweka vikwazo basi kumbuka faida hizi
Usiache kusubscribe at http://paulreuben59.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

The court system during colonialism in Tanzania.

Introduction. Pre-colonial Period Administration of justice during this time depended heavily on the social economic and political organization of the society in Tanganyika. Two systems of administration of justice namely; The Centralized and the Non-Centralized systems could be identified at the time. The Centralized Systems was applicable to societies with chiefs who played both roles of adjudicators and that of governors. In the Non-Centralized systems the entire community took part in the adjudication of disputes. However in both systems there were no formalization of procedure in adjudication, the customs of the respective societies prevailed in the process. Colonial Period The German Colonial Period. The Land currently covering Tanzania Main Land, was then included in what was called the German East Africa, it was subjected to the German Colonial Rule from 1886 up to the end of the First Ward War, 1918. During this Germany Colonial Rule the Administration of Justi...

Ndege ya Ukraine yaanguka Iran ikiwa na abiria 180, Abiria wote wafariki

Ndege ya Ukraine aina ya Boeing-737 iliyokuwa na abiria 180 imeanguka Iran, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo. Watoa huduma wa msalaba mwekundu wa Iran wanasema kuwa hakuna dalili yeyote kama kuna mtu aliyepona katika ajali hiyo. Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la kimataifa la ndege la Ukraine ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari katika uwanja wa ndege wa Imam Khomeini mjini Tehran. Ripoti za awali zinadai kuwa ndege hiyo ilikuwa safarini kuelekea mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.  Haijabainika ikiwa ajali hiyo ina uhusiano wowote na mzozo wa Iran-na Marekani. Kikosi cha uokoaji tayari kimetumwa katika eneo la tukio karibu na uwanja wa ndege, eneo ambalo ndege lilianguka. Credit: GettyImage " Ndege imeshika moto na tumetuma kikosi huko ... ," kiongozi wa huduma za dharura Pirhossein Koulivand,ameviambia vyombo vya habari ambapo Reuters imeripoti. Je tutegemee machafuko zaidi kutokea? Endelea kuwa pamoja nasi bega kwa bega, mshirikishe na mwenz...